Pages

Showing posts with label Kitaifa. Show all posts
Showing posts with label Kitaifa. Show all posts

Friday, 3 June 2016

Manji aivimbia TFF na Baraza la Michezo


Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Yanga anayemaliza muda wake, Yusuf Manji, amegomea mchakato wa awali wa uchaguzi ulioandaliwa na Baraza la Michezo Tanzania (BMT) na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Akizungumza jana kabla ya kuchukua fomu, alisema hawezi kwenda kuchukua fomu za uchaguzi TFF aliodai wanataka kumhujumu.

Akizungumza klabuni hapo, Manji alifichua hujuma mbalimbali zilizokuwa zikipangwa kumhujumu katika mchakato wa uchaguzi uliokuwa chini ya TFF.


Khatimu Naheka, Mwananchi

Fifa dismiss report of Gianni Infantino probe

  • Fifa denied on Friday reports in German media that president Gianni Infantino was under investigation for a possible ethics violation.

Fifa president Italian Gianni Infantino speaks during the second day of the 66th Fifa Congress at the Centro Banamex in Mexico City on May 13, 2016. Senegalese UN diplomat Fatma Samoura was named Fifa's new secretary general on Friday. PHOTO | ALFREDO ESTRELLA |  AFP

GENEVA

Fifa denied on Friday reports in German media that president Gianni Infantino was under investigation for a possible ethics violation.

Die Welt newspaper reported that Infantino had improperly ordered the destruction of the minutes of a Fifa executive committee meeting held at last month's congress in Mexico city.

Fifa spokeswoman Delia Fischer said the allegations were baseless.

"The email exchange that makes mention of the deletion of audio files refers to a copy of the original audio file of the meeting that was improperly stored on a local drive," she said.

"This mention does not refer to the officially archived audio file. That file exists and is properly saved at Fifa."

Tanzania yashuka nafasi saba viwango FIFA


TANZANIA imeshuka nafasi 7 katika viwango vya soka vinavyotolewa kila mwezi na Shirikisho la soka Duniani ‘FIFA’ huku Argentina ikiendelea kuongoza.

Mei mwaka huu Tanzania ilipanda hadi nafasi ya 129 kabla ya kuporomoka hadi nafasi ya 136, huku  Kenya ikishuka nafasi 13 kutoka nafasi ya 102 hadi 129 wakati Uganda ikibaki nafasi ya 72 katika viwango hivyo.

Orodha hiyo iliyotolewa jana na FIFA, ilionesha kuwa Uganda inaongoza ukanda wa Afrika Mashariki na kati ikifuatiwa na Rwanda iliyopo nafasi ya 103, Ethiopia 125, Sudan Kaskazini 128, Kenya, Tanzania na Sudan Kusini 157.

Pia orodha hiyo ilionesha nchi ya Ivory Coast inaongoza Afrika kwa kuwa nafasi ya 36, ikifuatiwa na Ghana iliyokuwa nafasi ya 37 na Senegal iliyoko nafasi ya 41.

FIFA ilitaja Argentina kuwa kinara wa viwango vya soka duniani ikifuatiwa na Ubelgiji na Colombia huku nchi ya Tonga, Somalia na Eritrea zikiwa za mwisho kwenye orodha hiyo.

Na Adam Mkwepu, Mtanzania

Thursday, 21 April 2016

Angalia Video ya baadhi ya matukio Mechi ya Yanga na Al Ahly



Azam nguvu zote Ligi Kuu, Kombe la Shirikisho


BAADA ya kutupwa nje ya michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika na Esperance ya Tunisia, kikosi cha Azam kimesema kwa sasa kinaelekeza nguvu zake kwenye michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara na ile ya Kombe la Shirikisho (FA).

Mabingwa hao wa Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, walijikuta wakitolewa na Esperance katika michuano hiyo ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa jumla ya mabao 4-2, baada ya juzi usiku kukubali kichapo cha mabao 3-0.

Azam FC wakicheza bila ya Pascal Wawa, Kipre Tchetche na Jean Batista Mugiraneza, walijikuta wanaruhusu mabao hayo 3-0 katika kipindi cha pili na kutolewa kwa matokeo ya jumla ya bao 4-2 kwani mchezo wa kwanza uliochezwa katika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar es Salaam, Wanalambalamba hao walifanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1.

Nahodha msaidizi wa kikosi hicho, Himid Mao, amewaambia mashabiki wao kuwa kwa sasa nguvu zao zote wanahamishia katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) na Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) akiwaahidi kuwa watapambana kuchukua makombe yote hayo mawili.

“Matokeo yamewasikitisha watu wengi hata sisi wachezaji, lakini wanatakiwa wajue Azam FC ni timu changa sana na kwa sasa tunapiga hatua kubwa lakini hii haitufanyi tuvimbe vichwa kwani bado tuna deni, hivyo nafikiri inabidi tufanye kitu kikubwa zaidi kuweza kusogea mbele.

“Mashabiki waendelee kutupa sapoti kwani bado ligi ipo, FA pia ipo hivyo tutajitahidi kuweza kuchukua makombe yote hayo,” alisema.

Kikosi hicho kinatarajiwa kuwasili nchini leo ambapo kitakwenda mkoani Shinyanga kucheza na Mwadui FC  mchezo wa nusu fainali michuano ya Kombe la Shirikisho (FA).

Azam FC iliyopanda Ligi Kuu miaka nane iliyopita, msimu huu ilikuwa ikishiriki kwa mara ya nne michuano ya Afrika hadi inafika raundi hiyo ilifanikiwa kuwatoa Bidvest Wits ya Afrika Kusini kwa jumla ya mabao 7-3.

Na Ezekiel Tendwa / Bingwa

Rafu yamwondoa Kessy Simba

  • Safari ya Azam, Yanga yanukia
  • Tippo adai watafanya biashara na timu yoyote


RAFU mbaya aliyoicheza beki mahiri wa Simba, Hassan Kessy dhidi ya mchezaji wa Toto African, Edward Christopher, imemsababishia kutemwa kuitumikia timu yake hiyo hadi mwisho wa msimu huu.

Kessy alimchezea rafu Christopher kwenye mchezo wao wa Ligi Kuu mwishoni mwa wiki iliyopita na kusababisha kutolewa nje kwa kadi nyekundu, huku uongozi wa Simba ukimuongezea adhabu ya kukosa michezo yote iliyobaki katika Ligi Kuu Tanzania Bara.

Mbali na kusimamishwa kwa mchezaji huyo, tayari kuna tetesi za kuikacha klabu hiyo na kujiunga na kati ya klabu ya matajiri wa Bongo, Azam au Watoto wa Jangwani, Yanga, licha ya tetesi hizo kutokuwekwa wazi.

Inadaiwa timu hizo Azam na Yanga zilikuwa zinasubiri kumalizika kwa michezo yao ya kimataifa ya marudiano kati ya timu za Esperance na Kombe la Shirikisho na Al Ahly mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, ili zianze mchakato wa kumnasa beki huyo ambaye mkataba wake unaisha mwezi Juni.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Kessy alisema bado uongozi haujampa taarifa zozote za kusimamishwa kwake.

“Sijapewa taarifa yoyote, lakini kama wameamua kunipa adhabu sawa nitaitumikia kwa kuwa bado ni mchezaji wao na bado nina mkataba nao, ila nikimaliza mkataba wangu mwezi wa sita meneja wangu ataamua kama nitabaki au nitaondoka,” alisema.

Kwa upande wa meneja wake Athuman Tippo, alisema wamepokea maamuzi ya uongozi huo kumsimamisha mchezaji wake na ataitumikia adhabu hiyo kama ilivyoamuliwa kwa kuwa ni mwajiriwa wao.

“Ataitumikia adhabu yake hadi atakapomaliza mkataba, lakini bado tunaendelea kusubiri adhabu watakayompa Vicent Angban na wasipofanya hivyo tutaendelea na msimamo wetu wa kuchukua hatua zaidi, tutakaa na mwanasheria na kupanga nini tufanye baada ya kipa huyo kujichukulia sheria mkononi kumpiga Kessy,” alisema.

Alisema hadi sasa bado hawajafanya mazungumzo na timu yoyote nyingine, lakini Kessy akimaliza mkataba wake atakuwa huru hivyo watafanya biashara na timu yoyote itakayomtaka.

Kessy jana alitangazwa na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba, Haji Manara, kuwa atakosa michezo yote iliyobaki katika ligi, akieleza alionekana kucheza rafu mbaya ambayo ingeweza kumsababishia kifo mchezaji huyo wa Toto.

“Kessy ameihujumu timu kwenye mchezo huo kwa rafu mbaya aliyoicheza, iliyosababisha kupewa kadi nyekundu kwani hakuwa na sababu ya kucheza vile alionekana kabisa ameinua mguu sijui ni makusudi au bahati mbaya, angeweza kumsababishia hata kifo Edward, hivyo tumeamua kumuongezea adhabu badala ya kukosa mechi mbili kwa kadi aliyopewa atazikosa mechi zote tano,” alisema.

Hata hivyo, mchezaji huyo mbali ya kucheza rafu hiyo iliyomuondoa Simba, alikuwa anaandamwa na jinamizi la kutoaminika tena Simba tangu alipoigharimu klabu yake katika mechi ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara, kati ya Simba na Yanga iliyochezwa Februari 20 kwa kuokoa mpira kizembe ambao ulinaswa na mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma na kufunga bao kirahisi.

Na Mwali Ibrahimu/ Mtanzania
Video : Mafoto

Saturday, 16 April 2016

Simba kushiriki michuano ya kimataifa


TIMU ya Simba imethibitisha kushiriki michuano ya Kombe la Nile Basin Championship, itakayoanza Mei 22 mwaka huu nchini Sudan.

Katika mashindano hayo mwaka huu, bingwa atajinyakulia zawadi ya dola za Kimarekani 30,000 sawa na Sh 65,697,000 huku mshindi wa pili akizawadiwa dola 20,000 (sawa na Sh 43,798,000 wakati mshindi wa tatu akipata dola za Kimarekani 10,000 (sawa na Sh 21,899,000).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Dar es Salaam jana na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), mashindano hayo hushirikisha timu zilizomaliza ligi zikiwa nafasi ya tatu na kwa kuwa Simba katika msimu uliopita ilimaliza Ligi Kuu Tanzania Bara katika nafasi hiyo, hivyo wamepewa jukumu la kuiwakilisha Tanzania katika mashindano hayo.

Mashindano ya Nile Basin yanashirikisha klabu kutoka katika nchi wanachama wa Cecafa ambazo ni Burundi, Djibouti, Ethiopia, Kenya, Sudan, Sudan Kusini, Tanzania Bara na Zanzibar

Kwa mara ya kwanza Tanzania iliwakilishwa na Mbeya City katika mashindano hayo yanayoandaliwa na Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) mwaka 2014, ambapo wakiwa chini ya kocha wao, Juma Mwambusi, ilijikuta ikiishia hatua ya robo fainali.

Mbeya City ilifanikiwa kuingia katika hatua hiyo ya robo fainali kwa jumla ya pointi 4 nafasi ya pili lakini ikajikuta ikitolewa na Victoria University kwa bao 1-0 ambaye pia ndiye bingwa mtetezi wa michuano hiyo kwa mwaka 2014 baada ya kuwafunga AFC Leopards ya Kenya kwa mabao 2-1 katika mchezo wa fainali.

NA ZAINAB IDDY/HABARI LEO

Yanga yarejea panapopendwa

Mfungaji wa bao pekee la Yanga katika mchezo wa jana, Simon Msuva.
TIMU ya soka ya Yanga jana ilimaliza mechi zake za viporo vyema kwa ushindi na kurejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara. Yanga iliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mtibwa Sugar Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, ikiwa ni mchezo wake wa mwisho wa viporo vyake vitatu ilivyokuwa navyo.

Jumatano Yanga iliifunga Mwadui ya Shinyanga mabao 2-1 katika uwanja huohuo na kabla ya hapo Yanga iliifunga pia Kagera Sugar mabao 3-1. Kutokana na matokeo ya jana, Yanga imefikisha pointi 59 na imechupa kutoka nafasi ya pili hadi ya kwanza ikiiengua Simba yenye pointi 57.

Timu zote zimecheza mechi 24. Hata hivyo Simba inaweza ikarejea kileleni tena leo kama itashinda mchezo wake wa raundi ya 25 dhidi ya Toto Africans utakaofanyika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Bao pekee la Yanga katika mchezo huo lilifungwa dakika ya 47 na Simon Msuva kwa shuti la mbali kutokana na mpira wa adhabu ndogo aliopasiwa na Haruna Niyonzima. Adhabu hiyo ilitokana na beki Andrew Vicent kumchezea madhambi Deus Kaseke wa Yanga.

Yanga itajilaumu kwa ushindi mwembamba kutokana na kupoteza nafasi kadhaa za kufunga, ambazo washambuliaji wake wakiongozwa na Donald Ngoma walishindwa kuzitumia.

Nayo Mtibwa ilipata nafasi za kufunga, lakini umaliziaji ulikuwa butu kwa kushindwa kulenga lango ama kupiga mipira dhaifu iliyodakwa na kipa Deogratias Munishi ‘Dida’. Kipigo hicho kimeifanya Mtibwa ibaki nafasi ya nne ikiwa na pointi 43 kwa michezo 26 iliyocheza.

Yanga sasa itaelekea nchini Misri kwa ajili ya kurudiana na Al Ahly Jumatano mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, ambapo mchezo wa kwanza uliofanyika Jumamosi wiki iliyopita Dar es Salaam timu hizo zilifungana bao 1-1. Yanga: Deogratius Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Oscar Joshua, Kevin Yondan/Malimi Busungu, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Vincent Bossou, Simon Msuva, Thabani Kamusoko, Donald Ngoma, Haruna Niyonzima na Deus Kaseke/ Amissi Tambwe.

Mtibwa Sugar: Said Mohamed, Ally Shomari, Majaliwa Shaaban, Andrew Vincent, Salim Mbonde/Boniface Maganga, Shaaban Nditi, Shiza Kichuya/ Vincent Barnabas, Muzamil Yassin, Ibrahim Rajab ‘Jeba’/Henry Joseph , Suleiman Rajab na Kelvin Friday.

NA MOHAMED AKIDA/ habari leo

Jose Mourinho tells pals he WILL be Manchester United boss this summer — and lines up Gonzalo Higuain swoop

  • The Special One explained to close friends and French giants PSG last week that he's Old Trafford bound and he wants Napoli's 32-goal striker to join him

Getting Higgy with it: Will Mourinho and Higuain be together at United next season?

Jose Mourinho is so adamant he will be Manchester United manager next season that he has lined up a move for £70million striker Gonzalo Higuain, writes Tom Hopkinson in the Sunday People.

Napoli rate Argentina international Higuain, who has already scored 32 goals for them this season, so highly they have slapped a £95m valuation on him.

But with only two years left on the 28-year-old's current deal, the Serie A title challengers are likely to drop the figure.

Former Chelsea, Real Madrid and Inter Milan boss Mourinho told French champions Paris Saint-Germain and close friends last week that he WILL take over at Old Trafford in the summer.

Louis van Gaal is not expected to hold onto the job, despite his side’s FA Cup quarter-final victory over West Ham.

And Mourinho is already working on targets, including Higuain and Benfica’s young midfield playmaker Renato Sanches.

The Special One was sacked for a second time by Chelsea owner Roman Abramovich in December.

But unlike the first time he was dismissed from Stamford Bridge, in 2007, his exit package did not contain a clause forbidding him to work for another English club within two seasons.

Mourinho said during that second spell at Chelsea that if Abramovich dismissed him again he would stay in England, and he has long harboured hopes of managing the Old Trafford giants.

Now he believes he has got his wish with Van Gaal’s roller-coaster two-year reign drawing to an end.

Mirror

Waamuzi waibana TFF


KAMATI ya Waamuzi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imesema kuwa haikubaliani na maamuzi ya Kamati ya Nidhamu ya kuwasimamisha waamuzi waliochezesha mechi za mwisho za Ligi Daraja la Kwanza kati ya JKT Kanembwa FC dhidi ya Geita Gold na Polisi Tabora dhidi ya JKT Oljoro.

Pia kamati hiyo ipo tayari kuwasaidia waamuzi hao waliosimamishwa wakituhumiwa kupanga matokeo iwapo watakuwa tayari kukata rufaa.

Akizungumza na MTANZANIA Jumamosi, Mwenyekiti wa Kamati ya Waamuzi, Salum Chama, alisema kuwa wakati suala hilo likifanyiwa uchunguzi na Kamati ya Nidhamu, hakuna mwamuzi yeyote mkongwe au aliyekuwepo katika kamati yao aliyeitwa ili kutafsiri mipaka na kanuni za kazi zao.

Alisema wao kamati ya waamuzi wamekuja kusikia maamuzi yakitolewa pasipo kushirikishwa jambo ambalo halipo kisheria lakini pia maamuzi yaliyotolewa hayakuwa na haki kwani hakuna ushahidi wa kutosha uliowakamatisha waamuzi hao.

“Kuanzia mwanzo hadi mwisho wa sakata lile hakuna aliyeshirikishwa katika kamati yetu, jambo ambalo kwa upande fulani si haki kwani na sisi tuna sheria na kanuni zetu ambazo tunazitumia uwanjani, lakini pia hadi hivi sasa hakuna ushahidi wa kutosha ni vipi wamekutwa na tuhuma za upangaji matokeo.

“Sisi kamati ya waamuzi, tupo tayari kuwasimamia bega kwa bega  iwapo kama wenyewe wanaona hawakutendewa haki na wakakata rufaa, lakini wakiomba tuwasimamie katika hilo tupo tayari,” alisema Chama.

Hivi karibuni Kamati ya Nidhamu ya TFF chini ya Makamu Mwenyekiti wake Wakili, Jerome Msemwa, iliwafungia maisha kutojihusisha na mpira wa miguu mwamuzi wa mchezo kati ya JKT Kanembwa FC v Geita Gold, Saleh Mang’ola, kamisaa wa mchezo huo, Moshi Juma pamoja na mwamuzi wa mchezo kati ya Polisi Tabora dhidi ya JKT Oljoro, Masoud Mkelemi na mwamuzi wa akiba, Fedian Machunde, waliofungiwa kwa muda wa miaka kumi  pamoja na kutozwa faini ya shilingi milioni kumi kila mmoja baada ya kukutwa na hatia ya upangaji matokeo kwenye michezo hiyo.

NA ZAINAB IDDY/ MTANZANIA

Wednesday, 6 April 2016

Takukuru yatua TFF

Ofisi za TFF jijini Dar es salaam.
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU), imesema inazo taarifa zote juu ya tuhuma za rushwa ndani ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na tayari imeanza uchunguzi.

Kwa zaidi ya mwezi sasa kumekuwa na tuhuma za rushwa ndani ya shirikisho hilo baada ya kumalizika kwa mechi za mwisho za Ligi Daraja la Kwanza Kundi C zilizohusisha timu za Geita Gold, Polisi Tabora, JKT Kanembwa na JKT Oljoro.

Suala hilo limeifanya Kamati ya Nidhamu ya TFF kuwafungia maisha na kuwasimamisha kwa miaka kumi baadhi ya viongozi wa soka na wachezaji.

Aidha baada ya adhabu hiyo, juzi kwenye mitandao ya kijamii zilisambaa sauti zinazodaiwa kuwa za baadhi ya viongozi wa TFF wakipanga matokeo ya moja ya mechi hizo.

Akizungumza na gazeti hili jana, msemaji wa Takukuru, Tunu Mleli, alisema taarifa wanazo na wanazifanyia kazi.

“Ndiyo taarifa tunazo na tumeshaanza uchunguzi.. ile ‘clip’ (ya sauti za wanaodaiwa viongozi wa TFF kupanga matokeo) imetufikia na tunaitumia kwenye uchunguzi wetu, lakini siwezi kusema utakamilika lini kwa sababu uchunguzi ni jambo endelevu na lipo kisheria zaidi, kwa hiyo tunachunguza ukishakamilika tutatoa taarifa,” alisema.

Kamati ya nidhamu ya TFF chini ya Makamu Mwenyekiti wake, Jerome Msemwa iliwafungia kujihusisha na soka maisha viongozi saba wa mchezo huo kwa kuhusishwa na upangaji matokeo katika mechi za Kundi C.

Mbali na kufungiwa kwa viongozi hao kamati hiyo pia imefungia wachezaji wawili na waamuzi wawili kujihusisha na soka kwa miaka 10 kila mmoja huku wakipigwa faini ya Sh milioni 10 kila mmoja.

Aidha, kamati hiyo imezishusha mpaka daraja la pili timu za Geita Gold, iliyokuwa ipande Ligi Kuu, JKT Oljoro ya Arusha na Polisi Tabora, huku JKT Kanembwa ya Kigoma ikishushwa mpaka hatua ya ligi ya mkoa (RCL). Kanembwa ilishika nafasi ya mwisho katika kundi na tayari ilishashuka daraja.

Waliofungiwa maisha ni Mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoa wa Tabora (Tarefa), Yusuph Kitumbo na Katibu wake, Fateh Rhemtullah, Mwenyekiti wa JKT Oljoro, Amos Mwita na kocha msaidizi wa Polisi Tabora, Bernard Fabian.

Wengine waliofungiwa maisha ni mwamuzi wa mchezo kati ya JKT Kanembwa FC na Geita Gold, Saleh Mang’ola, Kamisaa wa mchezo huo, Moshi Juma na kocha msaidizi wa Geita Gold, Choki Abeid.

Kwa upande wa wachezaji waliofungiwa miaka 10 ni kipa Mohammed Mohammed wa JKT Kanembwa na Dennis Richard wa Geita Gold huku wakitakiwa kulipwa faini ya Sh milioni 10 kila mmoja.

Kally Ongala atamba kuiua Coastal Union Ligi Kuu

Kocha Mkuu wa Majimaji ya Songea, Kalimangonga `Kally’ Ongala

KOCHA Mkuu wa timu ya Majimaji ya Songea, Kalimangonga `Kally’ Ongala amesema timu yake imejiandaa kuifunga Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaofanyika leo Uwanja wa Majimaji.

Akizungumza na gazeti hili jana kwa njia ya simu, Ongala alisema wachezaji wake watapambana sana kushinda mechi zao zote zilizobaki wakianza dhidi ya Coastal ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kukwepa janga la kushuka daraja.

“Wachezaji wote wako salama, hatuna majeruhi yeyote lakini mechi ya kesho (leo) ni mechi ngumu na tunahitaji kila mchezaji awe makini sana kwani haitakuwa mechi rahisi kwa sababu Coastal nayo iko katika hali mbaya, itahitaji kujikwamua,” alisema Ongala, kocha msaidizi wa zamani wa Azam FC.

Majimaji ipo katika nafasi ya 10 ikiwa na pointi 27 ilizovuna katika michezo wakati Coastal inaburuza mkia miongoni mwa timu 16, ikiwa na pointi 19 tu baada ya kucheza mechi 25.

Baada ya mchezo dhidi ya Coastal, Majimaji itasafiri hadi Mwanza kuumana na Toto African ya huko Jumatatu ijayo.

Habari Leo

Yanga: Kambi Pemba itatoa majibu Jumamosi


UONGOZI wa klabu ya Yanga umeeleza kuwa kambi waliyoweka visiwani Pemba itawasaidia kuibuka na ushindi katika mchezo wa kwanza wa hatua ya 16 bora wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al Ahly.

Yanga inatarajia kuvaana na Al Ahly, ambao ni vinara wa Ligi Kuu nchini Misri, katika mchezo utakaochezwa Jumamosi hii katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kambi hiyo imeonekana kuwa na mafanikio kwa Yanga, ikumbukwe kambi hiyo ndio iliyomtia adabu Mnyama Simba kuangukia pua katika michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara katika mzunguko wa kwanza na wa pili.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Ofisa Habari wa klabu hiyo, Jerry Muro, alisema matokeo hayo wanayoyatarajia, yatakuja baada ya Yanga kuwa na maandalizi mazuri Pemba kuelekea kwenye mechi dhidi ya Waarabu hao wa Misri.

“Tumeamua kwenda huko kwa kuwa ni sehemu tulivu na mara nyingi tumekuwa tukipata matokeo mazuri tukitokea huko, hivyo tunarajia kupata ushindi.

“Tulipata shida sana, lakini tuliweza kusafiri jana (juzi) na sasa tupo Pemba, wachezaji wataendelea na mazoezi yao kama kawaida tukijiandaa  na ushindi dhidi ya Al Ahly,” alisema Muro.

NA ADAM MKWEPU, MTANZANIA
Yanga ina ari ya kushinda mchezo wa kwanza hapa nyumbani, ili kujiwekea mazingira mazuri ikiwa ugenini.

Sunday, 27 March 2016

CAF: Chad yajiondoa Tz mashakani


Chad imejiondoa kutoka kwenye kinyang'anyiro cha kufuzu kwa dimba la mataifa ya Afrika linalotarajiwa kufanyika mwakani huko Gabon.

Shirikisho la soka la Chad limefikia kauli hiyo kutokana na ukosefu wa fedha.

Katika barua iliyotumwa kwa shirikisho la soka la Tanzania,mwenyekiti wa shirikisho la soka la Chad Moctar Mahamoud, alisema kuwa hawana fedha za kutosha kufadhili safari ya kwenda Dar Salaam kwa mechi ya marudiano dhidi ya Taifa Stars hapo kesho.

CAF imewapiga marufuku Chad kutoka kwenye mashindano ya mwaka wa 2019 mbali na kuitoza faini ya dola $20,000 pesa za Marekani.

Kufuati kujiondoa kwa Chad sasa matokeo ya mechi zote dhidi ya Chad zimefutiliwa mbali na shirikisho la soka la Afrika CAF.

Chad ilikuwa inaburuta mkia katika kundi G.

Tanzania iliyokuwa imeratibiwa kucheza mechi ya marudiano dhidi ya Chad kesho sasa imesalia na pointi 1.

Misri iliyokuwa imeizaba Chad 5-1 sasa ndio wanaongoza kundi hilo wakiwa na alama 4.

Super Eagles ya Nigeria ambao wameratibiwa kuchuana dhidi ya Misri mjini Alexandria siku ya Jumanne sasa sharti washinde alama zote ilikumaliza katika nafasi ya kwanza.

Sheria za CAF zinasema kuwa endapo kundi litakuwa na timu 3 basi timu inayoongoza pekee ndiyo inayosonga mbele.

BBC Swahili

Zlatan Ibrahimovic confirms Premier League interest ahead of potential summer move


The Swedish strike ace is out of contract at French side Paris Saint-Germain this summer and has been tipped for a final fling in England

Zlatan Ibrahimovic has admitted he is considering offers to move to the Premier League this summer.

Arsenal have been offered the 34-year-old Swedish superstar while Jose Mourinho will move for Ibrahimovic if he gets the Manchester United job.

Ibrahimovic is out of contract at Paris Saint-Germain this summer and fancies a move to England.

Sweden striker Ibrahimovic, talking ahead if a friendly with Czech Republic, said: "Yes, there is interest from the Premier League, I can confirm that.

"The Premier League is the league in the world all people and fans speak about.

"A lot of things have to feel fine when I'm going to take a decision this summer."

Manchester City and Chelsea could also be interested while Arsenal know Ibrahimovic - currently on around £300,000-a-week - fancies a club in London.

United would be in pole position if Mourinho is installed because the pair are very close and Ibrahimovic wants to link up with him.

Ubora, udhaifu Yanga, Azam kimataifa


Dar es salaam. Wakati Yanga na Azam zikijiandaa kukabiliana na vigogo vya soka Afrika kutoka kaskazini mwa bara hilo mwezi ujao, timu hizo zitabebwa au hata kuangushwa na washambuliaji, safu zao za ulinzi zinazohitaji marekebisho makubwa.

Yanga itacheza na Al Ahly ya Misri katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika utakaofanyika Aprili 9 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati Azam itaikabili Esperance ya Tunisia, Aprili 10 kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika (CAF) utakaochezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.

Msimu huu, timu hizo zimeonekana kuwa na safu kali ya ushambuliaji ambazo ni nadra kutoka uwanjani bila bao kwenye mchezo wowote, huku pia zikiwa na viungo mahiri wanaozibeba kwenye mashindano, lakini kama watakuwa kwenye ubora wao.

Yanga inabebwa na washambuliaji, Donald Ngoma, Amissi Tambwe, Simon Msuva na wengineo ambao wamefunga mabao 51 hadi sasa kwenye Ligi Kuu, wakati Azam inaongozwa nao, Kipre Tchetche, John Bocco, Farid Mussa walioiwezesha timu yao kufunga mabao 37.

Waonavyo wadau wa soka
Hata hivyo, baadhi ya wadau wa soka wamekiri kuwa timu hizo zinao uwezo wa kufanya vizuri, ila zinapaswa kurekebisha kasoro ndogo kwenye safu zao za ulinzi ambazo zikiachwa zitawagharimu katika michezo hiyo.

Kocha msaidizi wa JKT Ruvu, Mrage Kabange alisema Yanga na Azam zina soka la kiwango kikubwa, lakini wanapaswa kuongeza juhudi uwanjani katika michezo hiyo, huku wakiamini kila kitu kinawezekana.

Kabange aliyewahi kuichezea Simba na kuzinoa klabu kadhaa nchini alisema timu hizo hazipaswi kuwaogopa wapinzani wao kwani soka la sasa si kama lile zamani ambalo lilikuwa zaidi la mazoea.

Alizitaka klabu hizo kupambana ili kuhakikisha zinaibuka na ushindi katika michezo yao ya nyumbani, zikiamini kuwa ugenini lolote linaweza kutokea, ikiwamo fitina za Waarabu.

“Yanga na Azam zinao washambuliaji wazuri wanaoweza kufunga mabao muda wowote na ubora wa hizo timu unabebwa na aina ya washambuliaji wao, lakini zina matatizo kwenye upande wa mabeki.

“Ukiangalia Yanga, mabeki wake kwanza hawajiamini, wana tatizo la kujipanga, wana papara na wana tatizo kwenye ukabaji na hilo linaweza kuwaletea madhara kwani Waarabu hutakiwi kuwaachia wacheze.

“Pia, Azam nao wana matatizo kwenye upande wa mabeki, angalia hata mechi yao iliyopita dhidi ya Bidvest ya Afrika Kusini, mabeki walizembea, hivyo timu zote zinatakiwa kurekebisha hilo haraka,la sivyo itawagharimu,” alisema Kabange.

Mchezaji wa zamani wa Yanga ambaye kwa sasa ni mchambuzi wa masuala ya michezo, Ali Mayay alisema Yanga inapaswa kupunguza makosa katika safu yao ya ulinzi, huku akiwataka viungo kuongeza umakini.

“Yanga imekuwa na makosa makubwa katika ulinzi, mabeki wao wengi wamepunguza umakini, pia safu ya kiungo nayo inapoteza mipira, hivyo kama wasiporekebisha makosa hayo watapata matatizo mbele ya Waarabu,” alisema Mayay.

Mshambuliaji wa zamani wa Simba, Yanga na Taifa Stars, Zamoyoni Mogella au Golden Boy alisema Yanga na Azam, zote ni timu nzuri lakini zinatakiwa kuwa na nidhamu ya juu ya mchezo ziatakpopambana na Waarabu.

“Siwezi kusema sehemu gani zina upungufu kwani wachezaji wa timu hizo hawana nidhamu ya mchezo, angalia kama Yanga walipokuwa Rwanda walicheza vizuri walipokuja nyumbani mechi ya marudiano walicheza ovyo, sasa wakicheza hivyo mbele ya Waarabu itawagharimu.

“Uzoefu nilionao unapocheza na Waarabu unatakiwa kuwa na nidhamu, kwa sababu timu za huko zinakuadhibu kutokana na makosa unayofanya.

“Azam na Yanga zinatakiwa kuzidisha umakini uwanjani na kusaidiana kwani hata kama eneo fulani mfano ni zuri kama timu haina umakini litaonekana baya,” alisema Mogella.

Oliver Albert, Mwananchi

Thursday, 24 March 2016

Michezo ya kufuzu Afcon kuendelea

Kikosi cha Taifa la Ghana

Michezo ya kusaka tiketi ya kushiki michuano ya kombe la mataifa ya afrika mwaka 2017 itayofanyika Gabon itaendelea tena leo

Katika kundi A timu ya taifa ya Djibout itakua nyumbani katika uwanja wake wa Djibouty kukipiga na liberia.

Ghana maarufu kama the Black Stars walioko kundi H watakua wenyeji wa timu ya  Mozambique wanaofahamika kama Mambas.

Comoros watashuka dimbani kuwakabili Botswana huku Madagascar akipimana ubavu na timu ya taifa ya Jamuhuri ya Africa ya kati.

Bao la Samatta laibana Chad, Kenya yachapwa


Bao la Mshambulizi wa Taifa Stars lilitosha kuipa Tanzania ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Chad katika mechi ya kufuzu kwa kombe la mataifa ya Afrika.

Mkwaju wa Samatta kunako dakika ya 30 ya kipindi cha kwanza ilitosha kuipa Taifa Stars ushindi muhimu ugenini.

Kufuatia ushindi huo Taifa Stars ya Tanzania imeimarika na kutoshana nguvu na Nigeria inayoorodheshwa katika nafasi ya pili.

Chad nayo imetokomea ikiburuta mkia katika kundi hilo la G bila alama yeyote.

Nigeria hata hivyo imeratibiwa kuchuana dhidi ya vinara wa ligi hiyo Misri siku ya Ijumaa.
Katika kundi C, Benin ilisajili ushindi mkubwa wa amabao 2-1 ugenini dhidi ya wenyeji wao Sudan Kusini.

Mshambulizi wa klabu ya Uingereza ya West Brom Stephane Sessegnon, alifungua kivuno hicho kunako dakika ya 16 kabla ya kuhakikishia timu hiyo alama tatu muhimu zikiwa zimesalia robo saa mechi hiyo kukamilika.

Kufuatia ushindi huo Benin imejikita kileleni baada ya kuipiku Mali.

Mechi hiyo iliyochezewa Juba ilishuhudiwa na rais mpya wa FIFA Gianni Infantino.

Kenya kwa upande wake itajilaumu yenyewe baada ya kupoteza nafasi nzuri ya kuipiku Guinea nyumbani kwao iliposhindwa bao moja kwa nunge Ugenini.

Harambee Stars ya Kenya ambayo imebadilisha kocha, ilifika Guinea na wachezaji wa nyumbani kabla ya kujiunga na wachezaji wake wa kigeni siku ya mechi.

Kufuatia kichapo hicho Kenya ndio inayoburuta mkia katika kundi hilo bila ushindi wowote.
Vinara wa kundi hilo Zambia na Congo walitoka sare ya bao 1-1.

Katika mechi nyingine Sao Tome na Principe ilitoka nyuma na kuilaza Libya 2-1 katika kundi F.

BBC Swahili

Monday, 29 February 2016

Samatta aibeba Genk



Dar es Salaam. Mshambuliaji wa Kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta amefunga bao lake la kwanza Ulaya wakati timu yake Genk ikichapa Club Brugge kwa mabao 3-2 katika Ligi Kuu Ubelgiji.

Samatta aliyeingia akitokea benchi katika dakika 77, alitumia dakika nne tu kupachika bao lake la kwanza na kuihakikishia timu yake pointi tatu muhimu kwenye Uwanja wake wa nyumbani wa Cristal Arena. Hicho ni kipigo cha kwanza kwa vinara wa Ligi Kuu Ubelgiji, Club Brugge mwaka huu.

Club Brugge ilianza mchezo kwa kasi na kufanikiwa kupata bao la kuongoza kupitia Thomas Meunier, lakini Genk iliamka na kupata bao la kusawazisha kwa mkwaju wa penalti dakika 36 mfungaji akiwa na Nikolaos Karelis, kabla ya Thomas Buffel kuongeza la pili dakika ya 50.

Samatta alipachika bao la tatu kwa wenyeji katika dakika ya 81, Club Brugge ilipata bao la pili kupitia Hans Vanaken katika dakika 83.

Hata hivyo, siku hiyo nzuri ya Samatta iliingia doa baada ya kuonyeshwa kadi njano katika dakika ya 90.

Habari : Mwananchi
Picha na Video : Kwa msaada wa Mtandao

Simba yamalizia hasira Singida Utd

Mshambuliaji wa Simba, Brian Majwega akikwepa mguu wa mchezaji wa Singida United, Ponzi Mgeni wakati wa mechi yao ya Kombe la Shirikisho kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam jana.

SIMBA jana ilimaliza hasira za kufungwa na Yanga kwa Singida United baada ya kuichapa mabao 5-1 na kutinga hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la FA.

Mechi hiyo ni ya kwanza kwa Simba tangu itoke kupokea kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa mtani wake Yanga katika mechi ya Ligi Kuu bara iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam Februari 20 mwaka huu.

Simba ilitawala asilimia kubwa ya mchezo wa jana tangu mwanzo wa kipindi cha kwanza na kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 2-0.

Dan Lyanga aliiandikia Simba bao la kuongoza katika dakika ya tatu kabla Hamisi Kiiza hajaongeza la pili katika dakika ya 21.

Kiiza alifunga bao hilo baada ya kipa wa Singida United, Jacton Munna kuanguka ambapo aliuwahi mpira na kuujaza wavuni.

Kiiza aliifungia Simba bao la tatu katika dakika ya 66 kwa kichwa baada ya kuunganisha pasi ya Brian Majwega. Bao la nne la Simba liliwekwa kimiani na Awadhi Juma katika dakika ya 83 na dakika tatu baadae alifunga bao la tano.

United ilipata bao la kufutia machozi katika dakika ya 90 likifungwa na Paul Malamla. Aidha Simba ingeweza kupata mabao mengi jana kama washambuliaji wake wangezidisha umakini kwani walikosa mabao ya wazi mfululizo.

Kiiza alikosa bao dakika ya 13 na Lyanga alikosa dakika ya 16 baada ya wote kupiga mipira nje wakiwa kwenye nafasi nzuri ya kufunga.

Kutoka kwenye uwanja wa CCM Kirumba Mwanza mwandishi Alexandra Sanga anaripoti wenyeji Toto Africans walishindwa kutumia vema uwanja wao baada ya kuchachapwa bao 1-0 na Geita Gold.

Bao la Geita lilifungwa na Chibuga Chibuga katika dakika ya 64 baada ya kupata pasi ya Juma Nade.

 GRACE MKOJERA / HABARI LEO