Pages

Wednesday, 6 April 2016

Kally Ongala atamba kuiua Coastal Union Ligi Kuu

Kocha Mkuu wa Majimaji ya Songea, Kalimangonga `Kally’ Ongala

KOCHA Mkuu wa timu ya Majimaji ya Songea, Kalimangonga `Kally’ Ongala amesema timu yake imejiandaa kuifunga Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaofanyika leo Uwanja wa Majimaji.

Akizungumza na gazeti hili jana kwa njia ya simu, Ongala alisema wachezaji wake watapambana sana kushinda mechi zao zote zilizobaki wakianza dhidi ya Coastal ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kukwepa janga la kushuka daraja.

“Wachezaji wote wako salama, hatuna majeruhi yeyote lakini mechi ya kesho (leo) ni mechi ngumu na tunahitaji kila mchezaji awe makini sana kwani haitakuwa mechi rahisi kwa sababu Coastal nayo iko katika hali mbaya, itahitaji kujikwamua,” alisema Ongala, kocha msaidizi wa zamani wa Azam FC.

Majimaji ipo katika nafasi ya 10 ikiwa na pointi 27 ilizovuna katika michezo wakati Coastal inaburuza mkia miongoni mwa timu 16, ikiwa na pointi 19 tu baada ya kucheza mechi 25.

Baada ya mchezo dhidi ya Coastal, Majimaji itasafiri hadi Mwanza kuumana na Toto African ya huko Jumatatu ijayo.

Habari Leo

Related Posts:

  • African Lyon yarejea Ligi Kuu Bara TIMU ya soka ya African Sports imerejea katika michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara licha ya kutoka sare ya bao 1-1 na Ashanti United, katika mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) uliochezwa jana katika Uwanja wa Karume, … Read More
  • Kocha Mbelgiji asema SAMATTA ana nafasi ya kufanya vizuri akiwa Ubelgiji. Samatta akiwa katika vyumba vya kubailishia nguo vya timu yake mpya ya Grenk Kocha bora wa michuano ya Kombe la Chalenji msimu uliopita, Adel Amrouche amesema mshambuliaji Mbwana Samatta ana nafasi ya kufanya vizuri ak… Read More
  • Simba yatakata TAIFA huku Yanga ikifungwa MKWAKWANI Simba leo imezidi kuwapa raha mashabiki wake baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4 - 0 dhidi ya African Sports uwanja wa Taifa Dar es salaam, huku Yanga ikilala kwa mabao 2 - 0 mbele ya Coastal Union uwanja wa Mkwakwani … Read More
  • Mayanja asuka mkakati kuimaliza Yanga KOCHA wa Simba, Jackson Mayanja, amesema anaandaa mbinu mpya ili aweze kuifunga Yanga katika mchezo wao wa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa Jumamosi hii katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. M… Read More
  • ‘Simba Tunataka ubingwa’ BEKI na Nahodha Msaidizi wa Simba, Hassan Isihaka amesema kwa sasa wanafanya vizuri katika Ligi Kuu Bara na mpaka wapinzani wao waje kushtuka tayari watakuwa kwenye ubingwa. Isihaka alisema kwa sasa Simba wanaota ubi… Read More

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here