Pages

Wednesday, 6 April 2016

Kally Ongala atamba kuiua Coastal Union Ligi Kuu

Kocha Mkuu wa Majimaji ya Songea, Kalimangonga `Kally’ Ongala

KOCHA Mkuu wa timu ya Majimaji ya Songea, Kalimangonga `Kally’ Ongala amesema timu yake imejiandaa kuifunga Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaofanyika leo Uwanja wa Majimaji.

Akizungumza na gazeti hili jana kwa njia ya simu, Ongala alisema wachezaji wake watapambana sana kushinda mechi zao zote zilizobaki wakianza dhidi ya Coastal ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kukwepa janga la kushuka daraja.

“Wachezaji wote wako salama, hatuna majeruhi yeyote lakini mechi ya kesho (leo) ni mechi ngumu na tunahitaji kila mchezaji awe makini sana kwani haitakuwa mechi rahisi kwa sababu Coastal nayo iko katika hali mbaya, itahitaji kujikwamua,” alisema Ongala, kocha msaidizi wa zamani wa Azam FC.

Majimaji ipo katika nafasi ya 10 ikiwa na pointi 27 ilizovuna katika michezo wakati Coastal inaburuza mkia miongoni mwa timu 16, ikiwa na pointi 19 tu baada ya kucheza mechi 25.

Baada ya mchezo dhidi ya Coastal, Majimaji itasafiri hadi Mwanza kuumana na Toto African ya huko Jumatatu ijayo.

Habari Leo

Related Posts:

  • Niyonzima rasmi Yanga Sakata la Niyonzima kufukuzwa Yanga limechukua mwezi mmoja kabla ya wiki iliyopita kumalizana na kiungo huyo kuomba radhi ili aweze kurejeshwa kikosini. Yanga ilitangaza kuvunja mkataba na Niyonzima kwa madai kwamba … Read More
  • Mayanja aula mfupa uliomshinda Kerr Dar es Salaam . Kocha wa Simba, Jackson Mayanja ameamua kucheza kamali iliyomshinda mtangulizi wake Dylan Kerr kwa kuamua kuwapa nafasi wachezaji Rafael Kiongera na Hassan Isihaka katika kikosi chake cha kwanza. … Read More
  • I wouldn't sign for Chelsea right now - and nor would any top player, says Thierry Henry Sticking the boot in: Henry doesn't believe Chelsea will attract top talent this month The Blues are unlikely to qualify for next season's Champions League and it is not yet known who will manage the club when Guus Hid… Read More
  • Simba yatakata TAIFA huku Yanga ikifungwa MKWAKWANI Simba leo imezidi kuwapa raha mashabiki wake baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4 - 0 dhidi ya African Sports uwanja wa Taifa Dar es salaam, huku Yanga ikilala kwa mabao 2 - 0 mbele ya Coastal Union uwanja wa Mkwakwani … Read More
  • Marseille yajitosa kumtaka Samatta Dar es Salaam. Wakati timu za Nantes na RCK Genk zikiendelea  kupigana vikumbo kwa ajili ya kuinasa saini ya mshambuliaji, Mbwana Samatta, klabu ya Olympique de Marseille nayo imejitosa kumuwania mshambuliaji huyo.… Read More

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here