Pages

Sunday, 3 January 2016

Ngonjera za uwanja Simba zafikia patamu


Dar es Salaam. Ngonjera kuhusu ujenzi wa uwanja wa kisasa wa klabu ya Simba zimehamia mwaka 2016, huku ikielezwa kuwa tayari klabu hiyo imepata mwekezaji. Uwanja huo ulioko Bunju, nje kidogo ya Dar es Salaam umegeuka hekaya za viongozi wa klabu hiyo kwa muda mrefu sasa.

Jana, kiongozi mwandamizi wa klabu hiyo aliliambia gazeti hili kuwa wapo katika hatua za mwisho za kusaini mkataba na mwekezaji huyo mzawa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa uwanja wao na ujenzi kupangwa kuanza rasmi mwishoni mwa mwezi.

Klabu hiyo, pia ilithibitisha kupata mwekezaji aliyetajwa kuwa ni Mtanzania na kwamba hadi kukamilika kwa uwanja huo utagharimu zaidi ya Sh2 bilioni.

Rais wa klabu hiyo, Evance Aveva hakuwa tayari kukubali wala kukanusha kufikiwa kwa hatua hiyo.

Awali, kiongozi huyo wa Simba alilithibitishia gazeti hili kuwa makubaliano baina ya pande hizo mbili yamefikia hatua nzuri.

Kiongozi huyo ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya utendaji ya klabu hiyo alisema mchakato wa kupata mwekezaji na ujenzi umefikia hatua ya makubaliano ambayo yako katika hatua za mwisho na wakati wowote mwezi huu ujenzi utaanza.

“Tayari, tumepata mwekezaji mzawa amekubali kujenga uwanja wetu na kwa kweli tuko katika hatua nzuri na niwaambie wapenzi na mashabiki wetu (Simba) hadi kufikia Januari 30, wataanza kuona mabadiliko kule Bunju,” alisema kiongozi huyo na kuongeza:
“Hadi kukamilika ramani yetu ya mwanzo ilionyesha tutatumia sh2bilioni, lakini huenda ikapungua au kuongezeka, itajulikana rasmi karibuni ni kiasi gani tutatumia, lakini awali ilikuwa Sh2 bilioni.”

Mohammed Dewji
Kuhusu uwekezaji wa mfanyabiashara maarufu, Mohamed Dewji (MO) ambaye amekuwa akitajwa kuitaka klabu hiyo , kiongozi huyo alisema suala lake halikuwa rasmi, bali mazungumzo ya pembeni.

“Mo hakuja rasmi kwetu, alikuwa akizungumza pembeni, hivyo, hatukuwa na sababu ya kusikiliza vitu ambavyo si rasmi, alibainisha kiongozi huyo.

Aveva alipoulizwa kuhusu MO, alisema aachwe apumzike kipindi hiki cha sikukuu.

Wakati huo huo, suala la kocha msaidizi wa timu yao, baada ya kuondoka kwa Seleman Matola, jukumu hilo limeachwa kwa kocha mkuu, Dylan Kerr.

Uongozi wa klabu hiyo umeeleza kutokuwa tayari kumwingilia kocha huyo na kusisitiza kuwa atakapokuwa tayari yeye ndiye ataupa uongozi taarifa za kocha aliyempata.

Ushindi wa juzi wa Simba dhidi ya Ndanda umempa Kerr aliyeuelezea kuwa umempa nguvu ya kutetea taji kwenye mashindano ya Kombe la Mapinduzi Zanzibar, ambako timu hiyo itakata utepe na Jamhuri ya Pemba kesho usiku.

Imani Makongoro/ Mwananchi

Related Posts:

  • Mayanja asuka mkakati kuimaliza Yanga KOCHA wa Simba, Jackson Mayanja, amesema anaandaa mbinu mpya ili aweze kuifunga Yanga katika mchezo wao wa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa Jumamosi hii katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. M… Read More
  • ‘Simba Tunataka ubingwa’ BEKI na Nahodha Msaidizi wa Simba, Hassan Isihaka amesema kwa sasa wanafanya vizuri katika Ligi Kuu Bara na mpaka wapinzani wao waje kushtuka tayari watakuwa kwenye ubingwa. Isihaka alisema kwa sasa Simba wanaota ubi… Read More
  • Marseille yajitosa kumtaka Samatta Dar es Salaam. Wakati timu za Nantes na RCK Genk zikiendelea  kupigana vikumbo kwa ajili ya kuinasa saini ya mshambuliaji, Mbwana Samatta, klabu ya Olympique de Marseille nayo imejitosa kumuwania mshambuliaji huyo.… Read More
  • Simba yatakata TAIFA huku Yanga ikifungwa MKWAKWANI Simba leo imezidi kuwapa raha mashabiki wake baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4 - 0 dhidi ya African Sports uwanja wa Taifa Dar es salaam, huku Yanga ikilala kwa mabao 2 - 0 mbele ya Coastal Union uwanja wa Mkwakwani … Read More
  • Kocha Mbelgiji asema SAMATTA ana nafasi ya kufanya vizuri akiwa Ubelgiji. Samatta akiwa katika vyumba vya kubailishia nguo vya timu yake mpya ya Grenk Kocha bora wa michuano ya Kombe la Chalenji msimu uliopita, Adel Amrouche amesema mshambuliaji Mbwana Samatta ana nafasi ya kufanya vizuri ak… Read More

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here