Pages

Monday, 8 February 2016

‘Simba Tunataka ubingwa’


BEKI na Nahodha Msaidizi wa Simba, Hassan Isihaka amesema kwa sasa wanafanya vizuri katika Ligi Kuu Bara na mpaka wapinzani wao waje kushtuka tayari watakuwa kwenye ubingwa.

Isihaka alisema kwa sasa Simba wanaota ubingwa tu, hakuna jambo jingfine na kusema kuwa kwa kipindi chote tangu ameanza kuichezea Simba miaka minne iliyopita, inamuuma kuukosa ubingwa na kinachomshangaza, walikuwa wanacheza vizuri ila waliangushwa na bahati.

“Imani yangu ni kwamba msimu huu tutawafuta machozi mashabiki wa Simba kutokana na namna tunavyopata matokeo mazuri tunavyoshinda, maana awali, tulikuwa kama hatuna bahati kila tulipopambana hali ilikuwa ngumu.” Isihaka alisema na kuongeza:“Binafsi ninachokiamini, kufanya kwetu vizuri kasi yetu ni hadi tuchukue ubingwa, kama unavyojua wengine tangu tujiunge, Simba haijawahi kuchukua ubingwa huu.” 

Kuhusu wapinzani wao Yanga na Azam, beki huyo wa kati alisema wala hawaangalii wanafanya nini, akili zao kufanya yao ili kutimiza lengo la kutwaa ubingwa tu

Mwanaspoti

Related Posts:

  • Simba yavunja Mkataba na Makocha wake Simba sports club Dar es salaam 12-1-2016 Taarifa kwa vyombo vya habari Kwa masikitiko makubwa klabu ya Simba inawaarifu umma kupitia vyombo vya habari uamuzi wake wa kuvunja mikataba yake na makocha wake kocha … Read More
  • ‘Simba Tunataka ubingwa’ BEKI na Nahodha Msaidizi wa Simba, Hassan Isihaka amesema kwa sasa wanafanya vizuri katika Ligi Kuu Bara na mpaka wapinzani wao waje kushtuka tayari watakuwa kwenye ubingwa. Isihaka alisema kwa sasa Simba wanaota ubi… Read More
  • Mayanja aanza vizuri na Simba Kocha Jackson Mayanja ameanza vyema kibarua chake Simba, baada ya kuiongoza timu hiyo kuichapa Mtibwa Sugar bao 1-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mshambuliaji Hamis Kiiza aliifungia Simba bao hilo pekee kati… Read More
  • Mayanja aula mfupa uliomshinda Kerr Dar es Salaam . Kocha wa Simba, Jackson Mayanja ameamua kucheza kamali iliyomshinda mtangulizi wake Dylan Kerr kwa kuamua kuwapa nafasi wachezaji Rafael Kiongera na Hassan Isihaka katika kikosi chake cha kwanza. … Read More
  • Simba yatakata TAIFA huku Yanga ikifungwa MKWAKWANI Simba leo imezidi kuwapa raha mashabiki wake baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4 - 0 dhidi ya African Sports uwanja wa Taifa Dar es salaam, huku Yanga ikilala kwa mabao 2 - 0 mbele ya Coastal Union uwanja wa Mkwakwani … Read More

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here