Pages

Monday, 8 February 2016

‘Simba Tunataka ubingwa’


BEKI na Nahodha Msaidizi wa Simba, Hassan Isihaka amesema kwa sasa wanafanya vizuri katika Ligi Kuu Bara na mpaka wapinzani wao waje kushtuka tayari watakuwa kwenye ubingwa.

Isihaka alisema kwa sasa Simba wanaota ubingwa tu, hakuna jambo jingfine na kusema kuwa kwa kipindi chote tangu ameanza kuichezea Simba miaka minne iliyopita, inamuuma kuukosa ubingwa na kinachomshangaza, walikuwa wanacheza vizuri ila waliangushwa na bahati.

“Imani yangu ni kwamba msimu huu tutawafuta machozi mashabiki wa Simba kutokana na namna tunavyopata matokeo mazuri tunavyoshinda, maana awali, tulikuwa kama hatuna bahati kila tulipopambana hali ilikuwa ngumu.” Isihaka alisema na kuongeza:“Binafsi ninachokiamini, kufanya kwetu vizuri kasi yetu ni hadi tuchukue ubingwa, kama unavyojua wengine tangu tujiunge, Simba haijawahi kuchukua ubingwa huu.” 

Kuhusu wapinzani wao Yanga na Azam, beki huyo wa kati alisema wala hawaangalii wanafanya nini, akili zao kufanya yao ili kutimiza lengo la kutwaa ubingwa tu

Mwanaspoti

Related Posts:

  • Jonesia kuamua Simba na Yanga MWAMUZI Jonesia Rukiyaa wa mkoani Kagera, amepewa jukumu la kuchezesha mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga, katika mchezo wao unaotarajiwa kuchezwa  Jumamosi hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mwamuzi huyo m… Read More
  • ‘Simba Tunataka ubingwa’ BEKI na Nahodha Msaidizi wa Simba, Hassan Isihaka amesema kwa sasa wanafanya vizuri katika Ligi Kuu Bara na mpaka wapinzani wao waje kushtuka tayari watakuwa kwenye ubingwa. Isihaka alisema kwa sasa Simba wanaota ubi… Read More
  • Simba yamalizia hasira Singida Utd Mshambuliaji wa Simba, Brian Majwega akikwepa mguu wa mchezaji wa Singida United, Ponzi Mgeni wakati wa mechi yao ya Kombe la Shirikisho kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam jana. SIMBA jana ilimaliza hasira za kufung… Read More
  • Makocha watambiana ZIKIWA zimesalia siku tatu kabla ya pambano la watani wa jadi Simba na Yanga, makocha wa timu hizo wameonesha kuogopana huku kila mmoja akidai kuheshimu kikosi cha mwenziwe. Yanga imejichimbia Pemba na Simba imejichi… Read More
  • Mayanja asuka mkakati kuimaliza Yanga KOCHA wa Simba, Jackson Mayanja, amesema anaandaa mbinu mpya ili aweze kuifunga Yanga katika mchezo wao wa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa Jumamosi hii katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. M… Read More

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here