Pages

Wednesday, 17 February 2016

Jonesia kuamua Simba na Yanga


MWAMUZI Jonesia Rukiyaa wa mkoani Kagera, amepewa jukumu la kuchezesha mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga, katika mchezo wao unaotarajiwa kuchezwa  Jumamosi hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mwamuzi huyo mwenye beji ya Fifa, anaingia uwanjani kuzichezesha timu hizo kwa mara ya pili baada ya kuzihukumu katika mechi ya Nani Mtani Jembe 2014 ambao Simba iliibuka na ushindi wa bao 2-0.

Katika mchezo huo unaosubiriwa kwa hamu na mashabiki, Jonesia atasaidiana na Josephat Mburali (Tanga) na Samwel Mpenzu (Arusha), huku mwamuzi wa akiba akiwa ni Eli Kasihili wa Dar es Salaam,  wakati kamishna wa mchezo huo akiwa Khalid Mutego kutoka Mwanza.

Wakati huo huo, Shirikisho la Soka nchini (TFF), jana lilitangaza viingilio katika mchezo huo huku kiingilio cha chini kikiwa ni Sh 7,000.

Ofisa Habari wa TFF, Baraka Kizuguto, alisema kwa viti vya machungwa kiingilio kitakuwa  Sh 10,000 , VIP C na B ikiwa  ni Sh 20,000  huku VIP A ikiwa Sh 30,000.

Alisema tiketi zitaanza kuuzwa Ijumaa  katika vituo mbalimbali ikiwemo kwenye Ofisi za TFF Karume, Kidongo Chekundu, Uwanja wa Taifa, Dar Live, Buguruni sheli, Ubungo Oil Com, Steers, Feli na kituo cha mabasi Makumbusho.

Kizuguto aliwataka wadau pamoja na wapenzi wa mpira kununua tiketi hizo katika sehemu husika, ili kuepukana na matatizo ya kununua tiketi ambazo sio halali.

“Tunawaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi katika siku hiyo, ili kila mmoja aweze kuburudika na kushangilia timu yake ambapo ulinzi utakuwepo na umeimarika kwa kushirikiana na vyombo vya usalama,” alisema.

THERESIA GASPER, NA SUZANA MAKORONGO (RCT)
MTANZANIA

Related Posts:

  • Mayanja aula mfupa uliomshinda Kerr Dar es Salaam . Kocha wa Simba, Jackson Mayanja ameamua kucheza kamali iliyomshinda mtangulizi wake Dylan Kerr kwa kuamua kuwapa nafasi wachezaji Rafael Kiongera na Hassan Isihaka katika kikosi chake cha kwanza. … Read More
  • Mayanja aanza vizuri na Simba Kocha Jackson Mayanja ameanza vyema kibarua chake Simba, baada ya kuiongoza timu hiyo kuichapa Mtibwa Sugar bao 1-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mshambuliaji Hamis Kiiza aliifungia Simba bao hilo pekee kati… Read More
  • Simba yavunja Mkataba na Makocha wake Simba sports club Dar es salaam 12-1-2016 Taarifa kwa vyombo vya habari Kwa masikitiko makubwa klabu ya Simba inawaarifu umma kupitia vyombo vya habari uamuzi wake wa kuvunja mikataba yake na makocha wake kocha … Read More
  • Simba yatakata TAIFA huku Yanga ikifungwa MKWAKWANI Simba leo imezidi kuwapa raha mashabiki wake baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4 - 0 dhidi ya African Sports uwanja wa Taifa Dar es salaam, huku Yanga ikilala kwa mabao 2 - 0 mbele ya Coastal Union uwanja wa Mkwakwani … Read More
  • ‘Simba Tunataka ubingwa’ BEKI na Nahodha Msaidizi wa Simba, Hassan Isihaka amesema kwa sasa wanafanya vizuri katika Ligi Kuu Bara na mpaka wapinzani wao waje kushtuka tayari watakuwa kwenye ubingwa. Isihaka alisema kwa sasa Simba wanaota ubi… Read More

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here