Pages

Wednesday, 17 February 2016

Jonesia kuamua Simba na Yanga


MWAMUZI Jonesia Rukiyaa wa mkoani Kagera, amepewa jukumu la kuchezesha mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga, katika mchezo wao unaotarajiwa kuchezwa  Jumamosi hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mwamuzi huyo mwenye beji ya Fifa, anaingia uwanjani kuzichezesha timu hizo kwa mara ya pili baada ya kuzihukumu katika mechi ya Nani Mtani Jembe 2014 ambao Simba iliibuka na ushindi wa bao 2-0.

Katika mchezo huo unaosubiriwa kwa hamu na mashabiki, Jonesia atasaidiana na Josephat Mburali (Tanga) na Samwel Mpenzu (Arusha), huku mwamuzi wa akiba akiwa ni Eli Kasihili wa Dar es Salaam,  wakati kamishna wa mchezo huo akiwa Khalid Mutego kutoka Mwanza.

Wakati huo huo, Shirikisho la Soka nchini (TFF), jana lilitangaza viingilio katika mchezo huo huku kiingilio cha chini kikiwa ni Sh 7,000.

Ofisa Habari wa TFF, Baraka Kizuguto, alisema kwa viti vya machungwa kiingilio kitakuwa  Sh 10,000 , VIP C na B ikiwa  ni Sh 20,000  huku VIP A ikiwa Sh 30,000.

Alisema tiketi zitaanza kuuzwa Ijumaa  katika vituo mbalimbali ikiwemo kwenye Ofisi za TFF Karume, Kidongo Chekundu, Uwanja wa Taifa, Dar Live, Buguruni sheli, Ubungo Oil Com, Steers, Feli na kituo cha mabasi Makumbusho.

Kizuguto aliwataka wadau pamoja na wapenzi wa mpira kununua tiketi hizo katika sehemu husika, ili kuepukana na matatizo ya kununua tiketi ambazo sio halali.

“Tunawaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi katika siku hiyo, ili kila mmoja aweze kuburudika na kushangilia timu yake ambapo ulinzi utakuwepo na umeimarika kwa kushirikiana na vyombo vya usalama,” alisema.

THERESIA GASPER, NA SUZANA MAKORONGO (RCT)
MTANZANIA

Related Posts:

  • Yanga yarejea panapopendwa Mfungaji wa bao pekee la Yanga katika mchezo wa jana, Simon Msuva. TIMU ya soka ya Yanga jana ilimaliza mechi zake za viporo vyema kwa ushindi na kurejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara. Yanga iliibuka … Read More
  • Ubora, udhaifu Yanga, Azam kimataifa Dar es salaam. Wakati Yanga na Azam zikijiandaa kukabiliana na vigogo vya soka Afrika kutoka kaskazini mwa bara hilo mwezi ujao, timu hizo zitabebwa au hata kuangushwa na washambuliaji, safu zao za ulinzi zinazohit… Read More
  • Yanga yatangaza raha WAWAKILISHI wa Tanzania Bara katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Yanga, leo wataikabili Cercle de Joachim ya Mauritius ukiwa ni mchezo wa marudiano hatua ya awali. Katika mchezo wa kwanza ugenini Uwanja wa Ge… Read More
  • Makocha watambiana ZIKIWA zimesalia siku tatu kabla ya pambano la watani wa jadi Simba na Yanga, makocha wa timu hizo wameonesha kuogopana huku kila mmoja akidai kuheshimu kikosi cha mwenziwe. Yanga imejichimbia Pemba na Simba imejichi… Read More
  • Jonesia kuamua Simba na Yanga MWAMUZI Jonesia Rukiyaa wa mkoani Kagera, amepewa jukumu la kuchezesha mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga, katika mchezo wao unaotarajiwa kuchezwa  Jumamosi hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mwamuzi huyo m… Read More

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here