Pages

Sunday, 24 January 2016

Mayanja aula mfupa uliomshinda Kerr


Dar es Salaam . Kocha wa Simba, Jackson Mayanja ameamua kucheza kamali iliyomshinda mtangulizi wake Dylan Kerr kwa kuamua kuwapa nafasi wachezaji Rafael Kiongera na Hassan Isihaka katika kikosi chake cha kwanza.

Kauli ya Mayanja imekuja wakati mashabiki wa klabu hiyo wakilalamikia kiwango cha Kiongera aliyerudishwa kwenye usajili wa dirisha dogo kuwa ni cha chini na hapaswi kupewa nafasi.

Isihaka amekuwa akilaumiwa kwa kushuka kiwango na mara kwa mara hunyooshewa kidole kuwa kuwa uzembe wake umekuwa ukiigharimu Simba.

Hata hivyo, Mayanja amedai kukoshwa na viwango cha wachezaji hao na ameahidi kuwa ataendelea kuwapa nafasi kwa sababu wanafanya kazi ambayo huwatuma.

Mayanja alisema haoni sababu kwa wachezaji hao kulaumiwa kwa sababu yeye kama kocha ndiye anayefahamu ubora na uwezo wa mchezaji mmoja mmoja kiufundi na siyo mashabiki.

“Isihaka amecheza mechi mbili mfululizo na hatujaruhusu bao na sioni tatizo lolote kutoka kwake.

Pia, Kiongera naamini ana kitu kikubwa kwa sababu anasaidia kuipeleka timu mbele sifa ambayo mshambuliaji anatakiwa kuwa nao.

Bado ni wachezaji ninaowaamini na wakiendelea kufanya vizuri nitazidi kuwapa nafasi,” alisema Mayanja.

Mayanja alisema kuwa falsafa yake ni wachezaji kuzingatia kile anachowaelekeza na yeye binafsi hawezi kuingia kwenye mkumbo wa kupangiwa kikosi na mtu yeyote<

 Charles Abel/Mwananchi

Related Posts:

  • Jonesia kuamua Simba na Yanga MWAMUZI Jonesia Rukiyaa wa mkoani Kagera, amepewa jukumu la kuchezesha mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga, katika mchezo wao unaotarajiwa kuchezwa  Jumamosi hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mwamuzi huyo m… Read More
  • ‘Simba Tunataka ubingwa’ BEKI na Nahodha Msaidizi wa Simba, Hassan Isihaka amesema kwa sasa wanafanya vizuri katika Ligi Kuu Bara na mpaka wapinzani wao waje kushtuka tayari watakuwa kwenye ubingwa. Isihaka alisema kwa sasa Simba wanaota ubi… Read More
  • Mayanja asuka mkakati kuimaliza Yanga KOCHA wa Simba, Jackson Mayanja, amesema anaandaa mbinu mpya ili aweze kuifunga Yanga katika mchezo wao wa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa Jumamosi hii katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. M… Read More
  • Mayanja aula mfupa uliomshinda Kerr Dar es Salaam . Kocha wa Simba, Jackson Mayanja ameamua kucheza kamali iliyomshinda mtangulizi wake Dylan Kerr kwa kuamua kuwapa nafasi wachezaji Rafael Kiongera na Hassan Isihaka katika kikosi chake cha kwanza. … Read More
  • Simba yatakata TAIFA huku Yanga ikifungwa MKWAKWANI Simba leo imezidi kuwapa raha mashabiki wake baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4 - 0 dhidi ya African Sports uwanja wa Taifa Dar es salaam, huku Yanga ikilala kwa mabao 2 - 0 mbele ya Coastal Union uwanja wa Mkwakwani … Read More

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here