Pages

Sunday, 24 January 2016

Mayanja aula mfupa uliomshinda Kerr


Dar es Salaam . Kocha wa Simba, Jackson Mayanja ameamua kucheza kamali iliyomshinda mtangulizi wake Dylan Kerr kwa kuamua kuwapa nafasi wachezaji Rafael Kiongera na Hassan Isihaka katika kikosi chake cha kwanza.

Kauli ya Mayanja imekuja wakati mashabiki wa klabu hiyo wakilalamikia kiwango cha Kiongera aliyerudishwa kwenye usajili wa dirisha dogo kuwa ni cha chini na hapaswi kupewa nafasi.

Isihaka amekuwa akilaumiwa kwa kushuka kiwango na mara kwa mara hunyooshewa kidole kuwa kuwa uzembe wake umekuwa ukiigharimu Simba.

Hata hivyo, Mayanja amedai kukoshwa na viwango cha wachezaji hao na ameahidi kuwa ataendelea kuwapa nafasi kwa sababu wanafanya kazi ambayo huwatuma.

Mayanja alisema haoni sababu kwa wachezaji hao kulaumiwa kwa sababu yeye kama kocha ndiye anayefahamu ubora na uwezo wa mchezaji mmoja mmoja kiufundi na siyo mashabiki.

“Isihaka amecheza mechi mbili mfululizo na hatujaruhusu bao na sioni tatizo lolote kutoka kwake.

Pia, Kiongera naamini ana kitu kikubwa kwa sababu anasaidia kuipeleka timu mbele sifa ambayo mshambuliaji anatakiwa kuwa nao.

Bado ni wachezaji ninaowaamini na wakiendelea kufanya vizuri nitazidi kuwapa nafasi,” alisema Mayanja.

Mayanja alisema kuwa falsafa yake ni wachezaji kuzingatia kile anachowaelekeza na yeye binafsi hawezi kuingia kwenye mkumbo wa kupangiwa kikosi na mtu yeyote<

 Charles Abel/Mwananchi

Related Posts:

  • African Lyon yarejea Ligi Kuu Bara TIMU ya soka ya African Sports imerejea katika michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara licha ya kutoka sare ya bao 1-1 na Ashanti United, katika mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) uliochezwa jana katika Uwanja wa Karume, … Read More
  • Yanga yatangaza raha WAWAKILISHI wa Tanzania Bara katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Yanga, leo wataikabili Cercle de Joachim ya Mauritius ukiwa ni mchezo wa marudiano hatua ya awali. Katika mchezo wa kwanza ugenini Uwanja wa Ge… Read More
  • Mayanja asuka mkakati kuimaliza Yanga KOCHA wa Simba, Jackson Mayanja, amesema anaandaa mbinu mpya ili aweze kuifunga Yanga katika mchezo wao wa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa Jumamosi hii katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. M… Read More
  • Jonesia kuamua Simba na Yanga MWAMUZI Jonesia Rukiyaa wa mkoani Kagera, amepewa jukumu la kuchezesha mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga, katika mchezo wao unaotarajiwa kuchezwa  Jumamosi hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mwamuzi huyo m… Read More
  • Makocha watambiana ZIKIWA zimesalia siku tatu kabla ya pambano la watani wa jadi Simba na Yanga, makocha wa timu hizo wameonesha kuogopana huku kila mmoja akidai kuheshimu kikosi cha mwenziwe. Yanga imejichimbia Pemba na Simba imejichi… Read More

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here