Pages

Sunday, 24 January 2016

Mourinho hakutuma ombi la kazi Man Utd


Ripoti inayodai kuwa aliyekuwa meneja wa Chelsea,Jose Mourinho aliiandika Manchester United barua yenye kurasa sita akielezea upungufu wa kocha wa Man United Louis van Gaal imetajwa kuwa "ajabu kabisa", anasema wakala wake, Jorge Mendes.

Jarida la Independent la Jumapili pia limedai Mourinho aliwasilisha "uchambuzi wa kisayansi" wa kikosi kizima cha Old Trafford katika kile kinachoitwa " barua ya upendo" kwa klabu hiyo.

United walizomewa na mashabiki wao wa nyumbani hapo jana Jumamosi baada ya kulazwa bao 1-0 dhidi ya Southampton.

Mourinho, 52, hana kazi haswa baada ya kutimuliwa na Chelsea katika wa Desemba kufuatia matokeo duni.

Mendes alisema dhana ya kuwa Mreno huyo aliandika barua hiyo ilikuwa "ujinga".

Katika taarifa fupi: Mendez alisema "hamuoni kuwa kocha mwenye hadhi kama ya Mourinho hawezi kujidunisha kwa kuandikia vilabu nyaraka za kuomba kazi ?''

Baada ya kichapo hicho Old Trafford, vijana wa Van Gaal walizomewa sana na mashabiki .
Kilichowaaudhi sana ni takwimu kuwa Manchester United ilijifurukuta na kushambulia lango la wapinzani wao mara moja pekee katika mechi hiyo.

Van Gaal alinukuliwa akikiri kuwa yeye pamoja na vijana wake hawakufanya vyema katika mechi hiyo na kuwa walistahili kubezwa na kutupiwa matusi makali na mashabiki.

United wako katika nafasi ya 5 katika jedwali la ligi kuu ya Uingereza ikiwa na jumla ya alama 37.

Timu hiyo inahitaji zaidi ya alama 5 ilikunusuru nafasi nne za kwanza zitakayoiwezesha kushiriki katika ligi ya mabingwa barani Ulaya.

Alama hizo 37 ni za chini zaidi katika hiztoria ya klabu hiyo maarufu duniani baada ya kucheza mechi 23.

BBC Swahili

Related Posts:

  • Wenger : Ushindi dhidi ya City umetupa tumaini Meneja wa Arsenal Arsene wenger amefichua kuwa ushindi dhidi ya Man city imepiga jeki imani wanayohitaji katika mbio za kutwaa ligi ya Uingereza msimu huu. Arsenal haijawahi kunyanyua taji hilo tangu mwaka wa 2004.… Read More
  • LVG : Naweza kuondoka mwenyewe Man United Kocha wa Manchester United Louis van Gaal amesema kuwa anaweza "kujiuzulu mwenyewe" baada ya Stoke City kuwapiga magoli 2-0 katika kichapo chao cha nne mfululizo katika michuano yote. Mholanzi huyo, ambaye anakabiliw… Read More
  • Pellegrini: Aguero atarudi kutamba Meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini ameeleza matumaini yake kwamba Sergio Aguero ataanza kufunga tena mabao. Mshambuliaji huyo wa miaka 27 kutoka Argentina aliwafungia City bao la ushindi wakati wa ushindi wa… Read More
  • Kocha Julio aitishia Simba Kocha wa Mwadui FC ya Shinyanga, Jamhuri Kihwelo 'Julio' Ushindi wa magoli 2-1walioupata Mwadui FC dhidi ya Ndanda FC umemtia kiburi kocha Jamuhuri Kiwhelo na kusema Simba wajiandae na kipigo kwenye mchezo wao wa Jumam… Read More
  • Van Gaal: Hakuna muujiza wa kuokoa Man Utd Meneja wa Manchester United Louis van Gaal amesema hakuna muujiza wa kuimarisha hali ya klabu hiyo na lazima wahusika wote watie bidii. United wamecheza mechi nane bila kushinda hata moja, sita zikiwa ligini, na kush… Read More

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here