Pages

Monday, 15 February 2016

African Lyon yarejea Ligi Kuu Bara


TIMU ya soka ya African Sports imerejea katika michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara licha ya kutoka sare ya bao 1-1 na Ashanti United, katika mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) uliochezwa jana katika Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

Matokeo hayo yameiwezesha timu hiyo kuongoza katika kundi A kutokana na pointi 29 walizojikusanyia huku Ashanti wakishika nafasi ya pili kwa kufikisha pointi 24.

Katika mchezo huo, African Lyon walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya tatu lililofungwa na Omary Abdallah kwa shuti kali.

Ashanti United walisawazisha dakika ya 50 kupitia kwa Mwini Ally ambaye alifanikiwa kuwatoka mabeki wa African Lyon na kuachia shuti lililojaa wavuni.

African Lyon imeungana na Ruvu Shooting kurejea Ligi Kuu baada ya kushuka daraja, huku Geita Gold ikipata nafasi ya kupanda daraja kwa mara ya kwanza baada ya kuongoza katika kundi C.

MSHAM NGOJWIKE/ MTANZANIA

Related Posts:

  • Simba yamalizia hasira Singida Utd Mshambuliaji wa Simba, Brian Majwega akikwepa mguu wa mchezaji wa Singida United, Ponzi Mgeni wakati wa mechi yao ya Kombe la Shirikisho kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam jana. SIMBA jana ilimaliza hasira za kufung… Read More
  • Makocha watambiana ZIKIWA zimesalia siku tatu kabla ya pambano la watani wa jadi Simba na Yanga, makocha wa timu hizo wameonesha kuogopana huku kila mmoja akidai kuheshimu kikosi cha mwenziwe. Yanga imejichimbia Pemba na Simba imejichi… Read More
  • African Lyon yarejea Ligi Kuu Bara TIMU ya soka ya African Sports imerejea katika michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara licha ya kutoka sare ya bao 1-1 na Ashanti United, katika mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) uliochezwa jana katika Uwanja wa Karume, … Read More
  • Jonesia kuamua Simba na Yanga MWAMUZI Jonesia Rukiyaa wa mkoani Kagera, amepewa jukumu la kuchezesha mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga, katika mchezo wao unaotarajiwa kuchezwa  Jumamosi hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mwamuzi huyo m… Read More
  • Yanga yatangaza raha WAWAKILISHI wa Tanzania Bara katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Yanga, leo wataikabili Cercle de Joachim ya Mauritius ukiwa ni mchezo wa marudiano hatua ya awali. Katika mchezo wa kwanza ugenini Uwanja wa Ge… Read More

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here