Pages

Sunday, 17 January 2016

Mayanja aanza vizuri na Simba


Kocha Jackson Mayanja ameanza vyema kibarua chake Simba, baada ya kuiongoza timu hiyo kuichapa Mtibwa Sugar bao 1-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mshambuliaji Hamis Kiiza aliifungia Simba bao hilo pekee katika dakika ya tano akiunganisha kwa kichwa krosi ya Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ na kumfanya Mayanja kutembea kifua mbele.

Ushindi huo umeifanya Simba kufikisha pointi 30 na kuziongezea presha Azam na Yanga zilizazoongoza ligi hiyo kwa sasa, huku wakishusha Mtibwa hadi nafasi nne.

Katika mchezo huo, Mtibwa ilionekana kuzidiwa na kushindwa kuhimili kasi ya mashambulizi ya washambuliaji wa Simba, lakini umakini mdogo wa Kiiza, Ajibu uliwanyima wenyeji hao nafasi ya kupata mabao mengi.

Kipindi cha pili, Mtibwa ilirudi kwa kasi na kufanya shambulizi kali dakika ya 52 baada ya Ibrahim Jeba kuambaa na mpira na kuachia shuti lililogonga mwamba na kurudi uwanjani na mabeki wa Simba kuokoa.

Kiungo Justice Majabvi wa Simba alionyeshwa kadi ya njano dakika ya 13, kwa kumchezea rafu Shiiza Kichuya, pia dakika ya 22 Henry Joseph wa Mtibwa alionyeshwa kadi ya njano kwa kumchezea rafu Peter Mwalyanzi.

Katika michezo mingine iliyochezwa jana, kocha Abdallah Kibadeni alishuhudia timu yake ya JKT Ruvu ikipokea kipigo cha mabao 5-1 kutoka kwa Mgambo JKT.

Stand United ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Kagera Sugar, shukrani kwa goli lililofungwa na Revocatus Richard katika dakika ya 12.<

Coastal Union ililazimishwa sare 1-1 na Majimaji jijini Tanga. Coastal Union ilipata bao kupitia Absalim Chidiebele kabla ya Alex Kondo kuisawazishia Majimaji.

Jijini Mbeya wenyeji Mbeya City ilichapa Mwadui bao 1-0 lililofungwa na Ditram Nchimbi katika dakika ya 49, lakini         City ilipata pigo baada ya kiungo wake Haruna Moshi ‘Boban kuonyeshwa kadi nyekundu. Mshambuliaji Jeremia Juma aliingoza Prisons kuichapa Toto African bao 1-0 jijini Mwanza.

Related Posts:

  • Mayanja asuka mkakati kuimaliza Yanga KOCHA wa Simba, Jackson Mayanja, amesema anaandaa mbinu mpya ili aweze kuifunga Yanga katika mchezo wao wa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa Jumamosi hii katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. M… Read More
  • Makocha watambiana ZIKIWA zimesalia siku tatu kabla ya pambano la watani wa jadi Simba na Yanga, makocha wa timu hizo wameonesha kuogopana huku kila mmoja akidai kuheshimu kikosi cha mwenziwe. Yanga imejichimbia Pemba na Simba imejichi… Read More
  • Jonesia kuamua Simba na Yanga MWAMUZI Jonesia Rukiyaa wa mkoani Kagera, amepewa jukumu la kuchezesha mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga, katika mchezo wao unaotarajiwa kuchezwa  Jumamosi hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mwamuzi huyo m… Read More
  • ‘Simba Tunataka ubingwa’ BEKI na Nahodha Msaidizi wa Simba, Hassan Isihaka amesema kwa sasa wanafanya vizuri katika Ligi Kuu Bara na mpaka wapinzani wao waje kushtuka tayari watakuwa kwenye ubingwa. Isihaka alisema kwa sasa Simba wanaota ubi… Read More
  • Simba yatakata TAIFA huku Yanga ikifungwa MKWAKWANI Simba leo imezidi kuwapa raha mashabiki wake baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4 - 0 dhidi ya African Sports uwanja wa Taifa Dar es salaam, huku Yanga ikilala kwa mabao 2 - 0 mbele ya Coastal Union uwanja wa Mkwakwani … Read More

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here