Pages

Tuesday, 12 January 2016

Simba yavunja Mkataba na Makocha wake


Simba sports club
Dar es salaam
12-1-2016

Taarifa kwa vyombo vya habari

Kwa masikitiko makubwa klabu ya Simba inawaarifu umma kupitia vyombo vya habari uamuzi wake wa kuvunja mikataba yake na makocha wake kocha mkuu Dylan Kerr na kocha wake wa makipa Iddi Salim.

Katika uamuzi wake uliofanywa mchana huu na kikao cha kamati ya utendaji ambapo makocha hao waliitwa klabu ya Simba na walimu hao kwa pamoja wamekubaliana kuvunja mikataba ya ajira zao kwa faida ya pande zote mbili.

Kwa sasa kocha msaidizi wa Simba Jackson Mayanja atakuwa na timu huku mchakato wa kumpata kocha mkuu ukiendelea..

Mwisho uongozi unawashukuru walimu hao kwa huduma waliyoitoa katika kipindi chote cha uwepo wao klabuni.

Imetolewa na Haji S.Manara
Mkuu wa mawasiliano wa klabu ya Simba.
Simba nguvu moja

Related Posts:

  • Niyonzima rasmi Yanga Sakata la Niyonzima kufukuzwa Yanga limechukua mwezi mmoja kabla ya wiki iliyopita kumalizana na kiungo huyo kuomba radhi ili aweze kurejeshwa kikosini. Yanga ilitangaza kuvunja mkataba na Niyonzima kwa madai kwamba … Read More
  • Mayanja aula mfupa uliomshinda Kerr Dar es Salaam . Kocha wa Simba, Jackson Mayanja ameamua kucheza kamali iliyomshinda mtangulizi wake Dylan Kerr kwa kuamua kuwapa nafasi wachezaji Rafael Kiongera na Hassan Isihaka katika kikosi chake cha kwanza. … Read More
  • Mayanja aanza vizuri na Simba Kocha Jackson Mayanja ameanza vyema kibarua chake Simba, baada ya kuiongoza timu hiyo kuichapa Mtibwa Sugar bao 1-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mshambuliaji Hamis Kiiza aliifungia Simba bao hilo pekee kati… Read More
  • Samatta kuvuta mawakala wengi Tanzania BILA shaka kila mtu alisikia mshambuliaji wa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na timu ya Taifa ya Tanzania, Mbwana Samatta alishinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani. Ushindi wa… Read More
  • I wouldn't sign for Chelsea right now - and nor would any top player, says Thierry Henry Sticking the boot in: Henry doesn't believe Chelsea will attract top talent this month The Blues are unlikely to qualify for next season's Champions League and it is not yet known who will manage the club when Guus Hid… Read More

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here