Pages

Saturday, 2 January 2016

Yanga kunoa makali Kombe la Mapinduzi


TIMU ya Yanga tayari imewasili Zanzibar kwa ajili ya kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi itakayoanza kesho huku wakitamba kutwaa ubingwa na kusaka makali kwa ajili ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika.

Katika mashindano ya Mapinduzi, Yanga imepangwa kundi B ikiwa na Azam, Mtibwa Sugar na Mafunzo ya Zanzibar ambapo inatarajia kufungua dimba kesho kwa kuvaana na Mafunzo.

Kikosi hicho kinachonolewa na kocha Hans Vans Pluijm na msaidizi wake, Juma Mwambusi, tayari kipo visiwani Zanzibar.

Katika misimu ya hivi karibuni, Yanga wamekuwa wakilalamikiwa kutokana na kupeleka kikosi B lakini msimu huu wameamua kutuma kikosi kamili wakiwa na malengo ya kutwaa ubingwa pamoja na kuongeza ujuzi kwa ajili ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika.

Akizungumza kabla ya kuelekea Zanzibar, kocha Pluijm alisema kutokana na ugumu wa kundi walilopo ana imani kubwa utatoa changamoto kwa wachezaji wake ambao bado wana kazi kubwa ya kuhakikisha wanatetea ubingwa wa Tanzania Bara pamoja na kufanya vizuri katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika.

“Kikosi changu kamili kitakuwa Zanzibar na kila mchezaji atapangwa kulingana na uwezo wake atakaoonyesha kwenye mazoezi na baadhi ya mechi nimepanga kuwatumia wote kwani bado nina kazi kubwa mbele yangu.

“Nafikiri mashindano ya Mapinduzi yataongeza hali ya kimchezo kwa wachezaji wangu, kupitia mashindano hayo nitapata nafasi ya kuangalia mapungufu na kuyafanyia kazi na hii ni baada ya kukutana na timu ambazo hatujazizoea,” alisema.

Alisema baada ya Kombe la Mapinduzi kikosi chake kina kazi kubwa ya kujijenga ili kiweze kufanya vizuri katika kukabiliana na wapinzani wao, Cercle de Joachim ya Mauritius kwenye hatua ya kwanza ya mtoano wa michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika.

 NA ZAINAB IDDY, MTANZANIA

Related Posts:

  • Jonesia kuamua Simba na Yanga MWAMUZI Jonesia Rukiyaa wa mkoani Kagera, amepewa jukumu la kuchezesha mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga, katika mchezo wao unaotarajiwa kuchezwa  Jumamosi hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mwamuzi huyo m… Read More
  • Simba yatakata TAIFA huku Yanga ikifungwa MKWAKWANI Simba leo imezidi kuwapa raha mashabiki wake baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4 - 0 dhidi ya African Sports uwanja wa Taifa Dar es salaam, huku Yanga ikilala kwa mabao 2 - 0 mbele ya Coastal Union uwanja wa Mkwakwani … Read More
  • Yanga yatinga nusu fainali Mapinduzi Cup Mabingwa wa Tanzania Bara Timu ya Yanga, wamefanikiwa kutinga hatua ya Nusu fainali kufuatia ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mtibwa mabao ambayo yamefungwa na wachezaji Aboubakar na Malimi Busungu na kuwa kinara wa kundi … Read More
  • Mayanja asuka mkakati kuimaliza Yanga KOCHA wa Simba, Jackson Mayanja, amesema anaandaa mbinu mpya ili aweze kuifunga Yanga katika mchezo wao wa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa Jumamosi hii katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. M… Read More
  • Niyonzima rasmi Yanga Sakata la Niyonzima kufukuzwa Yanga limechukua mwezi mmoja kabla ya wiki iliyopita kumalizana na kiungo huyo kuomba radhi ili aweze kurejeshwa kikosini. Yanga ilitangaza kuvunja mkataba na Niyonzima kwa madai kwamba … Read More

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here