Pages

Sunday, 27 December 2015

Niyonzima asema hana furaha


KIUNGO mshambuliaji wa Yanga, Haruna Niyonzima amesema hana furaha kuwa nje ya Yanga na kuwataka mashabiki kuwa wavumilivu kwani suala lake linatarajiwa kupatiwa ufumbuzi hivi karibuni baada ya kuwasilisha maelezo yake kwa uongozi.

Akizungumza na gazeti la Habari leo juzi,  Niyonzima alisema Yanga ni timu yake na ameishi nayo vizuri pamoja na watu wake hivyo anaamini tofauti zao zitamazilika na kurejea kuitumikia.

“Yanga ni timu yangu na nimeishi nayo vizuri pamoja na watu wake, lakini sina furaha kwani nimekaa nje kwa muda usiojulikana lakini haya yote ni majaribu na najua ni vitu ambavyo vipo duniani ila naamini yataisha vizuri tu,” alisema.

“Mimi ni binadamu naweza kufanya makosa lakini nawahakikishia wapenzi wa Yanga na wa Niyonzima kwamba hili litaisha siku si nyingi na wataendelea kupata burudani kama ilivyokuwa na zaidi”.

Pia aliwatakia heri Yanga kwenye mchezo wa leo na heri ya Krismasi na Mwaka Mpya 2016 na kuwataka wamalize mwaka 2015 kwa amani. Niyonzima amesimamishwa kwa muda usiojulikana na uongozi wa Yanga kutokana na kuchelewa kurudi kujiunga na timu hiyo baada ya kumalizika kwa mashindano ya Chalenji iliyofanyika Ethiopia ambapo yeye alikuwa akiitumikia timu yake ya taifa ya Rwanda.

Related Posts:

  • Niyonzima aitishia nyau Yanga Dar es Salaam. Kiungo Haruna Niyonzima ameipa Yanga siku nne kubadili uamuzi wa kumfukuza na baada ya hapo ataanika ukweli wa mgogoro wake na klabu hiyo. Wakati Niyonzima akisema hayo, katibu mkuu wa Yanga, Dk Jonas … Read More
  • Niyonzima rasmi Yanga Sakata la Niyonzima kufukuzwa Yanga limechukua mwezi mmoja kabla ya wiki iliyopita kumalizana na kiungo huyo kuomba radhi ili aweze kurejeshwa kikosini. Yanga ilitangaza kuvunja mkataba na Niyonzima kwa madai kwamba … Read More
  • Niyonzima asema hana furaha KIUNGO mshambuliaji wa Yanga, Haruna Niyonzima amesema hana furaha kuwa nje ya Yanga na kuwataka mashabiki kuwa wavumilivu kwani suala lake linatarajiwa kupatiwa ufumbuzi hivi karibuni baada ya kuwasilisha maelezo yake … Read More
  • Yanga kunoa makali Kombe la Mapinduzi TIMU ya Yanga tayari imewasili Zanzibar kwa ajili ya kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi itakayoanza kesho huku wakitamba kutwaa ubingwa na kusaka makali kwa ajili ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika. Katika mash… Read More
  • Yanga yatinga nusu fainali Mapinduzi Cup Mabingwa wa Tanzania Bara Timu ya Yanga, wamefanikiwa kutinga hatua ya Nusu fainali kufuatia ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mtibwa mabao ambayo yamefungwa na wachezaji Aboubakar na Malimi Busungu na kuwa kinara wa kundi … Read More

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here