Pages

Sunday, 27 December 2015

Niyonzima asema hana furaha


KIUNGO mshambuliaji wa Yanga, Haruna Niyonzima amesema hana furaha kuwa nje ya Yanga na kuwataka mashabiki kuwa wavumilivu kwani suala lake linatarajiwa kupatiwa ufumbuzi hivi karibuni baada ya kuwasilisha maelezo yake kwa uongozi.

Akizungumza na gazeti la Habari leo juzi,  Niyonzima alisema Yanga ni timu yake na ameishi nayo vizuri pamoja na watu wake hivyo anaamini tofauti zao zitamazilika na kurejea kuitumikia.

“Yanga ni timu yangu na nimeishi nayo vizuri pamoja na watu wake, lakini sina furaha kwani nimekaa nje kwa muda usiojulikana lakini haya yote ni majaribu na najua ni vitu ambavyo vipo duniani ila naamini yataisha vizuri tu,” alisema.

“Mimi ni binadamu naweza kufanya makosa lakini nawahakikishia wapenzi wa Yanga na wa Niyonzima kwamba hili litaisha siku si nyingi na wataendelea kupata burudani kama ilivyokuwa na zaidi”.

Pia aliwatakia heri Yanga kwenye mchezo wa leo na heri ya Krismasi na Mwaka Mpya 2016 na kuwataka wamalize mwaka 2015 kwa amani. Niyonzima amesimamishwa kwa muda usiojulikana na uongozi wa Yanga kutokana na kuchelewa kurudi kujiunga na timu hiyo baada ya kumalizika kwa mashindano ya Chalenji iliyofanyika Ethiopia ambapo yeye alikuwa akiitumikia timu yake ya taifa ya Rwanda.

Related Posts:

  • Mayanja asuka mkakati kuimaliza Yanga KOCHA wa Simba, Jackson Mayanja, amesema anaandaa mbinu mpya ili aweze kuifunga Yanga katika mchezo wao wa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa Jumamosi hii katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. M… Read More
  • Simba yatakata TAIFA huku Yanga ikifungwa MKWAKWANI Simba leo imezidi kuwapa raha mashabiki wake baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4 - 0 dhidi ya African Sports uwanja wa Taifa Dar es salaam, huku Yanga ikilala kwa mabao 2 - 0 mbele ya Coastal Union uwanja wa Mkwakwani … Read More
  • Jonesia kuamua Simba na Yanga MWAMUZI Jonesia Rukiyaa wa mkoani Kagera, amepewa jukumu la kuchezesha mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga, katika mchezo wao unaotarajiwa kuchezwa  Jumamosi hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mwamuzi huyo m… Read More
  • Niyonzima rasmi Yanga Sakata la Niyonzima kufukuzwa Yanga limechukua mwezi mmoja kabla ya wiki iliyopita kumalizana na kiungo huyo kuomba radhi ili aweze kurejeshwa kikosini. Yanga ilitangaza kuvunja mkataba na Niyonzima kwa madai kwamba … Read More
  • Makocha watambiana ZIKIWA zimesalia siku tatu kabla ya pambano la watani wa jadi Simba na Yanga, makocha wa timu hizo wameonesha kuogopana huku kila mmoja akidai kuheshimu kikosi cha mwenziwe. Yanga imejichimbia Pemba na Simba imejichi… Read More

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here