Pages

Sunday, 27 March 2016

Kipa wa zamani wa Simba Dhaira amefariki


Aliyekuwa kipa nambari moja wa timu ya Simba na Uganda Abel Dhaira ameaga dunia.
Dhaira mwenye umri wa miaka 28 alikuwa anaugua saratani.

Dr. Bernard Ogwel, wa shirikisho la soka nchini Uganda FUFA ameithibitishia BBC kuwa kipa huyo alivuta pumzi yake ya mwisho akiwa Iceland.

"Ni jambo la kuhuzunisha sana kuwa Dhaira ametuacha kwetu kama waganda na pia kwa Familia yake''

Dhaira alikuwa amejiunga na klabu ya IBV Vestmannaeyjar ya Iceland alipogunduliwa kuwa anaugua saratani katika miezi ya hivi karibuni.

Kipa huyo alianza kuichezea Uganda Cranes mwaka wa 2009 alipoisaidia timu hiyo kutwaa kombe la CECAFA Senior Challenge 2012.

Afya yake ilidhoofika Januari mwaka huu na akalazwa katika hospitali ya Nsambya kabla ya kurejea Iceland kwa matibabu zaidi.

Kocha wake wa IBV Vestmannaeyjar, Bjarni Johannsson alikuwa ameahidi kumsaidia kwa hali na mali wakati huu anapokabiliwa na maradhi.

Dhaira aliwahi kuichezea Express FC ya Uganda kabla ya kujiunga na AS Vita ya DR Congo na kisha Simba FC ya Tanzania.

BBC Swahili

Related Posts:

  • Simba yavunja Mkataba na Makocha wake Simba sports club Dar es salaam 12-1-2016 Taarifa kwa vyombo vya habari Kwa masikitiko makubwa klabu ya Simba inawaarifu umma kupitia vyombo vya habari uamuzi wake wa kuvunja mikataba yake na makocha wake kocha … Read More
  • ‘Simba Tunataka ubingwa’ BEKI na Nahodha Msaidizi wa Simba, Hassan Isihaka amesema kwa sasa wanafanya vizuri katika Ligi Kuu Bara na mpaka wapinzani wao waje kushtuka tayari watakuwa kwenye ubingwa. Isihaka alisema kwa sasa Simba wanaota ubi… Read More
  • Simba yatakata TAIFA huku Yanga ikifungwa MKWAKWANI Simba leo imezidi kuwapa raha mashabiki wake baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4 - 0 dhidi ya African Sports uwanja wa Taifa Dar es salaam, huku Yanga ikilala kwa mabao 2 - 0 mbele ya Coastal Union uwanja wa Mkwakwani … Read More
  • Mayanja aula mfupa uliomshinda Kerr Dar es Salaam . Kocha wa Simba, Jackson Mayanja ameamua kucheza kamali iliyomshinda mtangulizi wake Dylan Kerr kwa kuamua kuwapa nafasi wachezaji Rafael Kiongera na Hassan Isihaka katika kikosi chake cha kwanza. … Read More
  • Mayanja aanza vizuri na Simba Kocha Jackson Mayanja ameanza vyema kibarua chake Simba, baada ya kuiongoza timu hiyo kuichapa Mtibwa Sugar bao 1-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mshambuliaji Hamis Kiiza aliifungia Simba bao hilo pekee kati… Read More

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here