Pages

Wednesday, 6 April 2016

Takukuru yatua TFF

Ofisi za TFF jijini Dar es salaam.
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU), imesema inazo taarifa zote juu ya tuhuma za rushwa ndani ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na tayari imeanza uchunguzi.

Kwa zaidi ya mwezi sasa kumekuwa na tuhuma za rushwa ndani ya shirikisho hilo baada ya kumalizika kwa mechi za mwisho za Ligi Daraja la Kwanza Kundi C zilizohusisha timu za Geita Gold, Polisi Tabora, JKT Kanembwa na JKT Oljoro.

Suala hilo limeifanya Kamati ya Nidhamu ya TFF kuwafungia maisha na kuwasimamisha kwa miaka kumi baadhi ya viongozi wa soka na wachezaji.

Aidha baada ya adhabu hiyo, juzi kwenye mitandao ya kijamii zilisambaa sauti zinazodaiwa kuwa za baadhi ya viongozi wa TFF wakipanga matokeo ya moja ya mechi hizo.

Akizungumza na gazeti hili jana, msemaji wa Takukuru, Tunu Mleli, alisema taarifa wanazo na wanazifanyia kazi.

“Ndiyo taarifa tunazo na tumeshaanza uchunguzi.. ile ‘clip’ (ya sauti za wanaodaiwa viongozi wa TFF kupanga matokeo) imetufikia na tunaitumia kwenye uchunguzi wetu, lakini siwezi kusema utakamilika lini kwa sababu uchunguzi ni jambo endelevu na lipo kisheria zaidi, kwa hiyo tunachunguza ukishakamilika tutatoa taarifa,” alisema.

Kamati ya nidhamu ya TFF chini ya Makamu Mwenyekiti wake, Jerome Msemwa iliwafungia kujihusisha na soka maisha viongozi saba wa mchezo huo kwa kuhusishwa na upangaji matokeo katika mechi za Kundi C.

Mbali na kufungiwa kwa viongozi hao kamati hiyo pia imefungia wachezaji wawili na waamuzi wawili kujihusisha na soka kwa miaka 10 kila mmoja huku wakipigwa faini ya Sh milioni 10 kila mmoja.

Aidha, kamati hiyo imezishusha mpaka daraja la pili timu za Geita Gold, iliyokuwa ipande Ligi Kuu, JKT Oljoro ya Arusha na Polisi Tabora, huku JKT Kanembwa ya Kigoma ikishushwa mpaka hatua ya ligi ya mkoa (RCL). Kanembwa ilishika nafasi ya mwisho katika kundi na tayari ilishashuka daraja.

Waliofungiwa maisha ni Mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoa wa Tabora (Tarefa), Yusuph Kitumbo na Katibu wake, Fateh Rhemtullah, Mwenyekiti wa JKT Oljoro, Amos Mwita na kocha msaidizi wa Polisi Tabora, Bernard Fabian.

Wengine waliofungiwa maisha ni mwamuzi wa mchezo kati ya JKT Kanembwa FC na Geita Gold, Saleh Mang’ola, Kamisaa wa mchezo huo, Moshi Juma na kocha msaidizi wa Geita Gold, Choki Abeid.

Kwa upande wa wachezaji waliofungiwa miaka 10 ni kipa Mohammed Mohammed wa JKT Kanembwa na Dennis Richard wa Geita Gold huku wakitakiwa kulipwa faini ya Sh milioni 10 kila mmoja.

PSG 2 - 2 Manchester City player ratings: Who was YOUR man of the match at the Parc des Princes?

  • Fernandinho took advantage of some poor PSG defending to net a vital second away goal as Manuel Pellegrini's men earned an impressive draw in Paris

All smiles: Manchester City players celebate their draw in Paris

Fernandinho hit a deflected equaliser as Manchester City snatched a 2-2 draw in the first leg of their Champions League quarter-final against Paris Saint-Germain.

City looked to be running into trouble at the Parc des Princes after casually allowing Zlatan Ibrahimovic to cancel out a Kevin De Bruyne strike and falling behind to an Adrien Rabiot tap-in.

But after Ibrahimovic continued to atone for an early penalty miss by heading against the bar, Fernandinho took advantage of some poor PSG defending to net a vital second away goal.

PSG

Trapp 5: Should have done better when beaten by De Bruyne’s powerful shot. Decent distribution.

Aurier 5: A few good deliveries from the right but at fault for City's second.

Thiago Silva 7: A class act, who loves to stride forward out of central defence and pick a pass.

Luiz 5: Cautioned within 12 seconds and failed to cut out pass for City goal. Won penalty though.

Maxwell 7: Bombed forward effectively down the left, positive-minded in the spirit of the night.

Thiago Motta 6: The man who makes things tick – but his passing wasn’t always accurate.

On target: Adrien Rabiot celebrates his goal

Rabiot 7: Opportunist’s strike to cap a lively performance in midfield.

Matuidi 5: Lost possession for De Bruyne goal and was wasteful on other occasions too.

Di Maria 8: Some sublime moments of skill and some very telling crosses from the Argentine.

Ibrahimovic 6: Missed penalty and another great chance – yet some of his contributions were majestic.

Cavani 7: Often excellent cutting in from the left, the Uruguayan is an intelligent team-player.

Subs: Lucas Moura (Rabiot 78), Van der Wiel (Aurier 78)



Man City

Hart 8: Brilliant penalty save, defied Ibrahimovic and kept City in with a shout.

Sagna 6: Conceded a penalty after sloppy defending which is most out of character.

Otamendi 5: An unconvincing performance as he was caught horribly in possession.

Mangala 5: Lucky not to concede a penalty when PSG were screaming for a push on Matuidi.

Clichy 5: Caught out of position, bombing forward when he should stay at home.

Fernandinho 7: Good display, solid defensively and scored City's second.

Leveller: Fernandinho levels for City

Fernando 4: Crazy moment of madness to gift Ibrahimovic an equaliser. Unforgivable error.

Silva 5: Glanced a header wide from a great chance. Below par season by his standards.

De Bruyne 7: What a difference his return has made. Superb finish and good all round quality.

Navas 6: One outstanding cross for Silva but does not offer enough to be in this team.

Aguero 7: Given very little service but still worked so hard, making countless runs.

Subs: Delph 77 (De Bruyne, Bony (Silva 88), Kolarov (Aguero 90)

Mirror

Kally Ongala atamba kuiua Coastal Union Ligi Kuu

Kocha Mkuu wa Majimaji ya Songea, Kalimangonga `Kally’ Ongala

KOCHA Mkuu wa timu ya Majimaji ya Songea, Kalimangonga `Kally’ Ongala amesema timu yake imejiandaa kuifunga Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaofanyika leo Uwanja wa Majimaji.

Akizungumza na gazeti hili jana kwa njia ya simu, Ongala alisema wachezaji wake watapambana sana kushinda mechi zao zote zilizobaki wakianza dhidi ya Coastal ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kukwepa janga la kushuka daraja.

“Wachezaji wote wako salama, hatuna majeruhi yeyote lakini mechi ya kesho (leo) ni mechi ngumu na tunahitaji kila mchezaji awe makini sana kwani haitakuwa mechi rahisi kwa sababu Coastal nayo iko katika hali mbaya, itahitaji kujikwamua,” alisema Ongala, kocha msaidizi wa zamani wa Azam FC.

Majimaji ipo katika nafasi ya 10 ikiwa na pointi 27 ilizovuna katika michezo wakati Coastal inaburuza mkia miongoni mwa timu 16, ikiwa na pointi 19 tu baada ya kucheza mechi 25.

Baada ya mchezo dhidi ya Coastal, Majimaji itasafiri hadi Mwanza kuumana na Toto African ya huko Jumatatu ijayo.

Habari Leo

Manchester United boss Louis van Gaal turns down Dutch FA job - so is he set to stay at Old Trafford?

  • The Dutch FA (KNVB) believed LVG could help reinvigorate the set up and restore Holland's credibility
          Rejection: Man United manager Louis van Gaal turned down a job offer from the Dutch FA

Manchester United manager Louis van Gaal has turned down the chance to become the KNVB's director of football.

But his decision to do so does not necessarily mean he will be staying on at Old Trafford beyond the end of this season, report the Manchester Evening News.

Van Gaal won the bronze medal at the 2014 World Cup in Brazil as Netherlands coach guiding them to third place at the finals. He returned from South America to officially take charge at United as David Moyes' successor on a three year deal.

While Van Gaal has had a fraught time in England the Netherlands have also suffered on the international stage since his departure for Old Trafford.

Old Trafford: Van Gaal's future is still unclear

Danny Blind's side were shock fallers in the Euro 2016 qualifiers and won't be in France for the summer tournament.

The Dutch FA believed LVG could help reinvigorate the set up and restore Holland's credibility. The Netherlands' top brass created the creator of football for Van Gaal and offered him the post.

Top job: Van Gaal with assistant manager Danny Blind during the 2014 World Cup

But during the international break from his United duties it is understood that the Reds boss turned down the opportunity.

It will fuel stories that the 64-year-old will be given the green light to go ahead and complete his three-year contract at Old Trafford.

Mirror

Yanga: Kambi Pemba itatoa majibu Jumamosi


UONGOZI wa klabu ya Yanga umeeleza kuwa kambi waliyoweka visiwani Pemba itawasaidia kuibuka na ushindi katika mchezo wa kwanza wa hatua ya 16 bora wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al Ahly.

Yanga inatarajia kuvaana na Al Ahly, ambao ni vinara wa Ligi Kuu nchini Misri, katika mchezo utakaochezwa Jumamosi hii katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kambi hiyo imeonekana kuwa na mafanikio kwa Yanga, ikumbukwe kambi hiyo ndio iliyomtia adabu Mnyama Simba kuangukia pua katika michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara katika mzunguko wa kwanza na wa pili.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Ofisa Habari wa klabu hiyo, Jerry Muro, alisema matokeo hayo wanayoyatarajia, yatakuja baada ya Yanga kuwa na maandalizi mazuri Pemba kuelekea kwenye mechi dhidi ya Waarabu hao wa Misri.

“Tumeamua kwenda huko kwa kuwa ni sehemu tulivu na mara nyingi tumekuwa tukipata matokeo mazuri tukitokea huko, hivyo tunarajia kupata ushindi.

“Tulipata shida sana, lakini tuliweza kusafiri jana (juzi) na sasa tupo Pemba, wachezaji wataendelea na mazoezi yao kama kawaida tukijiandaa  na ushindi dhidi ya Al Ahly,” alisema Muro.

NA ADAM MKWEPU, MTANZANIA
Yanga ina ari ya kushinda mchezo wa kwanza hapa nyumbani, ili kujiwekea mazingira mazuri ikiwa ugenini.