Pages

Thursday, 21 April 2016

Rafu yamwondoa Kessy Simba

  • Safari ya Azam, Yanga yanukia
  • Tippo adai watafanya biashara na timu yoyote


RAFU mbaya aliyoicheza beki mahiri wa Simba, Hassan Kessy dhidi ya mchezaji wa Toto African, Edward Christopher, imemsababishia kutemwa kuitumikia timu yake hiyo hadi mwisho wa msimu huu.

Kessy alimchezea rafu Christopher kwenye mchezo wao wa Ligi Kuu mwishoni mwa wiki iliyopita na kusababisha kutolewa nje kwa kadi nyekundu, huku uongozi wa Simba ukimuongezea adhabu ya kukosa michezo yote iliyobaki katika Ligi Kuu Tanzania Bara.

Mbali na kusimamishwa kwa mchezaji huyo, tayari kuna tetesi za kuikacha klabu hiyo na kujiunga na kati ya klabu ya matajiri wa Bongo, Azam au Watoto wa Jangwani, Yanga, licha ya tetesi hizo kutokuwekwa wazi.

Inadaiwa timu hizo Azam na Yanga zilikuwa zinasubiri kumalizika kwa michezo yao ya kimataifa ya marudiano kati ya timu za Esperance na Kombe la Shirikisho na Al Ahly mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, ili zianze mchakato wa kumnasa beki huyo ambaye mkataba wake unaisha mwezi Juni.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Kessy alisema bado uongozi haujampa taarifa zozote za kusimamishwa kwake.

“Sijapewa taarifa yoyote, lakini kama wameamua kunipa adhabu sawa nitaitumikia kwa kuwa bado ni mchezaji wao na bado nina mkataba nao, ila nikimaliza mkataba wangu mwezi wa sita meneja wangu ataamua kama nitabaki au nitaondoka,” alisema.

Kwa upande wa meneja wake Athuman Tippo, alisema wamepokea maamuzi ya uongozi huo kumsimamisha mchezaji wake na ataitumikia adhabu hiyo kama ilivyoamuliwa kwa kuwa ni mwajiriwa wao.

“Ataitumikia adhabu yake hadi atakapomaliza mkataba, lakini bado tunaendelea kusubiri adhabu watakayompa Vicent Angban na wasipofanya hivyo tutaendelea na msimamo wetu wa kuchukua hatua zaidi, tutakaa na mwanasheria na kupanga nini tufanye baada ya kipa huyo kujichukulia sheria mkononi kumpiga Kessy,” alisema.

Alisema hadi sasa bado hawajafanya mazungumzo na timu yoyote nyingine, lakini Kessy akimaliza mkataba wake atakuwa huru hivyo watafanya biashara na timu yoyote itakayomtaka.

Kessy jana alitangazwa na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba, Haji Manara, kuwa atakosa michezo yote iliyobaki katika ligi, akieleza alionekana kucheza rafu mbaya ambayo ingeweza kumsababishia kifo mchezaji huyo wa Toto.

“Kessy ameihujumu timu kwenye mchezo huo kwa rafu mbaya aliyoicheza, iliyosababisha kupewa kadi nyekundu kwani hakuwa na sababu ya kucheza vile alionekana kabisa ameinua mguu sijui ni makusudi au bahati mbaya, angeweza kumsababishia hata kifo Edward, hivyo tumeamua kumuongezea adhabu badala ya kukosa mechi mbili kwa kadi aliyopewa atazikosa mechi zote tano,” alisema.

Hata hivyo, mchezaji huyo mbali ya kucheza rafu hiyo iliyomuondoa Simba, alikuwa anaandamwa na jinamizi la kutoaminika tena Simba tangu alipoigharimu klabu yake katika mechi ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara, kati ya Simba na Yanga iliyochezwa Februari 20 kwa kuokoa mpira kizembe ambao ulinaswa na mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma na kufunga bao kirahisi.

Na Mwali Ibrahimu/ Mtanzania
Video : Mafoto

Saturday, 16 April 2016

These stats prove Marcus Rashford is ALREADY Manchester United's most important attacking player

  • The teenage sensation scored his seventh goal of the season against Aston Villa to continue a fantastic run since breaking into the first team

Marcus Rashford is having the season of his life.

Well, it is his first actual season as a top flight footballer, but the Manchester United starlet is absolutely smashing it since breaking into the first team.

He's already a huge hit with the Red Devils fans, not just for his goals but f or turning down Liverpool as a kid to wait for the nod from United.

And now he's one of - if not definitely - United's best striker. His latest goal was a clever finish against Aston Villa at Old Trafford, his seventh goal since his debut in February.

And thanks to Squawka Football there are some pretty damning stats that pretty much prove the 18-year-old is ALREADY United's best forward.

He's scored four goals from his last five shots, which is a stat Wayne Rooney and Anthony Martial can only dream of.

Also he's now scored as many goals in the first half of games at Old Trafford (3) as the rest of his team-mates.

And when compared to lowly Aston Villa's scoring exploits this season...well, there's only one winner.

Mirror

Simba kushiriki michuano ya kimataifa


TIMU ya Simba imethibitisha kushiriki michuano ya Kombe la Nile Basin Championship, itakayoanza Mei 22 mwaka huu nchini Sudan.

Katika mashindano hayo mwaka huu, bingwa atajinyakulia zawadi ya dola za Kimarekani 30,000 sawa na Sh 65,697,000 huku mshindi wa pili akizawadiwa dola 20,000 (sawa na Sh 43,798,000 wakati mshindi wa tatu akipata dola za Kimarekani 10,000 (sawa na Sh 21,899,000).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Dar es Salaam jana na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), mashindano hayo hushirikisha timu zilizomaliza ligi zikiwa nafasi ya tatu na kwa kuwa Simba katika msimu uliopita ilimaliza Ligi Kuu Tanzania Bara katika nafasi hiyo, hivyo wamepewa jukumu la kuiwakilisha Tanzania katika mashindano hayo.

Mashindano ya Nile Basin yanashirikisha klabu kutoka katika nchi wanachama wa Cecafa ambazo ni Burundi, Djibouti, Ethiopia, Kenya, Sudan, Sudan Kusini, Tanzania Bara na Zanzibar

Kwa mara ya kwanza Tanzania iliwakilishwa na Mbeya City katika mashindano hayo yanayoandaliwa na Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) mwaka 2014, ambapo wakiwa chini ya kocha wao, Juma Mwambusi, ilijikuta ikiishia hatua ya robo fainali.

Mbeya City ilifanikiwa kuingia katika hatua hiyo ya robo fainali kwa jumla ya pointi 4 nafasi ya pili lakini ikajikuta ikitolewa na Victoria University kwa bao 1-0 ambaye pia ndiye bingwa mtetezi wa michuano hiyo kwa mwaka 2014 baada ya kuwafunga AFC Leopards ya Kenya kwa mabao 2-1 katika mchezo wa fainali.

NA ZAINAB IDDY/HABARI LEO

Manchester City's Sergio Aguero rules out summer transfer back to Argentina — even if Blues lift the European Cup

  • "It's been said I would go home if I won the Champions League. But I’m not going to go. I have several years left here" vows striker PLUS: Kompany fitness latest
Blue blood: Aguero says he's staying at Manchester City for years to come

Sergio Aguero has no intention of quitting Manchester City.

Sunday Mirror Sport revealed last month that Etihad bosses expect to keep the Argentina international beyond a contract that still has three years still to run.

And now striker Aguero himself has confirmed that he has unfinished business with the Blues - even if they go on to lift the European Cup this season.

The 27-year-old, who has said he wants to one day rejoin boyhood club Independiente in Buenos Aires, said: “It has been said that I would go home if I won the Champions League.

“But I’m not going to go.

"I have several years left here and the Champions League is getting closer.

“I don’t know whether it will be this year or not, but the team is improving in Europe and it has always been the dream. We are growing and there will be a few more chances for me after this year.”

City face Spanish giants Real Madrid in the semi-finals - and Aguero admits it will be a tough ask after the way the Bernabeu side hit back from losing the away leg 2-0 to overcome Wolfsburg in the last round.

But he would love to face his former club Atletico Madrid, who face Bayern Munich and City's boss-to-be Pep Guardiola in the other semi, in the final in Milan next month.

Aguero said: “I wasn’t really surprised when our match with Paris Saint-Germain had finished to discover that Madrid had got past Wolfsburg — Real have very good players who can score a goal at any moment.

“I was hoping for the best for Atletico against Barca because they have been playing really well and Cholo (coach Diego Simeone) has had a great few years there.

"It makes me happy to see them doing well because Atleti will always be a special place for me because it was my first club in Europe.”

City skipper Vincent Kompany could make a return to the team for the trip to Newcastle on Tuesday after recovering from his latest calf strain.

But the Belgium international defender has told friends that he won’t be back up to full fitness until the first leg of the Champions League semi-finals on Wednesday week.

Mirror

Yanga yarejea panapopendwa

Mfungaji wa bao pekee la Yanga katika mchezo wa jana, Simon Msuva.
TIMU ya soka ya Yanga jana ilimaliza mechi zake za viporo vyema kwa ushindi na kurejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara. Yanga iliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mtibwa Sugar Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, ikiwa ni mchezo wake wa mwisho wa viporo vyake vitatu ilivyokuwa navyo.

Jumatano Yanga iliifunga Mwadui ya Shinyanga mabao 2-1 katika uwanja huohuo na kabla ya hapo Yanga iliifunga pia Kagera Sugar mabao 3-1. Kutokana na matokeo ya jana, Yanga imefikisha pointi 59 na imechupa kutoka nafasi ya pili hadi ya kwanza ikiiengua Simba yenye pointi 57.

Timu zote zimecheza mechi 24. Hata hivyo Simba inaweza ikarejea kileleni tena leo kama itashinda mchezo wake wa raundi ya 25 dhidi ya Toto Africans utakaofanyika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Bao pekee la Yanga katika mchezo huo lilifungwa dakika ya 47 na Simon Msuva kwa shuti la mbali kutokana na mpira wa adhabu ndogo aliopasiwa na Haruna Niyonzima. Adhabu hiyo ilitokana na beki Andrew Vicent kumchezea madhambi Deus Kaseke wa Yanga.

Yanga itajilaumu kwa ushindi mwembamba kutokana na kupoteza nafasi kadhaa za kufunga, ambazo washambuliaji wake wakiongozwa na Donald Ngoma walishindwa kuzitumia.

Nayo Mtibwa ilipata nafasi za kufunga, lakini umaliziaji ulikuwa butu kwa kushindwa kulenga lango ama kupiga mipira dhaifu iliyodakwa na kipa Deogratias Munishi ‘Dida’. Kipigo hicho kimeifanya Mtibwa ibaki nafasi ya nne ikiwa na pointi 43 kwa michezo 26 iliyocheza.

Yanga sasa itaelekea nchini Misri kwa ajili ya kurudiana na Al Ahly Jumatano mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, ambapo mchezo wa kwanza uliofanyika Jumamosi wiki iliyopita Dar es Salaam timu hizo zilifungana bao 1-1. Yanga: Deogratius Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Oscar Joshua, Kevin Yondan/Malimi Busungu, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Vincent Bossou, Simon Msuva, Thabani Kamusoko, Donald Ngoma, Haruna Niyonzima na Deus Kaseke/ Amissi Tambwe.

Mtibwa Sugar: Said Mohamed, Ally Shomari, Majaliwa Shaaban, Andrew Vincent, Salim Mbonde/Boniface Maganga, Shaaban Nditi, Shiza Kichuya/ Vincent Barnabas, Muzamil Yassin, Ibrahim Rajab ‘Jeba’/Henry Joseph , Suleiman Rajab na Kelvin Friday.

NA MOHAMED AKIDA/ habari leo