Pages

Wednesday, 6 April 2016

Kally Ongala atamba kuiua Coastal Union Ligi Kuu

Kocha Mkuu wa Majimaji ya Songea, Kalimangonga `Kally’ Ongala

KOCHA Mkuu wa timu ya Majimaji ya Songea, Kalimangonga `Kally’ Ongala amesema timu yake imejiandaa kuifunga Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaofanyika leo Uwanja wa Majimaji.

Akizungumza na gazeti hili jana kwa njia ya simu, Ongala alisema wachezaji wake watapambana sana kushinda mechi zao zote zilizobaki wakianza dhidi ya Coastal ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kukwepa janga la kushuka daraja.

“Wachezaji wote wako salama, hatuna majeruhi yeyote lakini mechi ya kesho (leo) ni mechi ngumu na tunahitaji kila mchezaji awe makini sana kwani haitakuwa mechi rahisi kwa sababu Coastal nayo iko katika hali mbaya, itahitaji kujikwamua,” alisema Ongala, kocha msaidizi wa zamani wa Azam FC.

Majimaji ipo katika nafasi ya 10 ikiwa na pointi 27 ilizovuna katika michezo wakati Coastal inaburuza mkia miongoni mwa timu 16, ikiwa na pointi 19 tu baada ya kucheza mechi 25.

Baada ya mchezo dhidi ya Coastal, Majimaji itasafiri hadi Mwanza kuumana na Toto African ya huko Jumatatu ijayo.

Habari Leo

Manchester United boss Louis van Gaal turns down Dutch FA job - so is he set to stay at Old Trafford?

  • The Dutch FA (KNVB) believed LVG could help reinvigorate the set up and restore Holland's credibility
          Rejection: Man United manager Louis van Gaal turned down a job offer from the Dutch FA

Manchester United manager Louis van Gaal has turned down the chance to become the KNVB's director of football.

But his decision to do so does not necessarily mean he will be staying on at Old Trafford beyond the end of this season, report the Manchester Evening News.

Van Gaal won the bronze medal at the 2014 World Cup in Brazil as Netherlands coach guiding them to third place at the finals. He returned from South America to officially take charge at United as David Moyes' successor on a three year deal.

While Van Gaal has had a fraught time in England the Netherlands have also suffered on the international stage since his departure for Old Trafford.

Old Trafford: Van Gaal's future is still unclear

Danny Blind's side were shock fallers in the Euro 2016 qualifiers and won't be in France for the summer tournament.

The Dutch FA believed LVG could help reinvigorate the set up and restore Holland's credibility. The Netherlands' top brass created the creator of football for Van Gaal and offered him the post.

Top job: Van Gaal with assistant manager Danny Blind during the 2014 World Cup

But during the international break from his United duties it is understood that the Reds boss turned down the opportunity.

It will fuel stories that the 64-year-old will be given the green light to go ahead and complete his three-year contract at Old Trafford.

Mirror

Yanga: Kambi Pemba itatoa majibu Jumamosi


UONGOZI wa klabu ya Yanga umeeleza kuwa kambi waliyoweka visiwani Pemba itawasaidia kuibuka na ushindi katika mchezo wa kwanza wa hatua ya 16 bora wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al Ahly.

Yanga inatarajia kuvaana na Al Ahly, ambao ni vinara wa Ligi Kuu nchini Misri, katika mchezo utakaochezwa Jumamosi hii katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kambi hiyo imeonekana kuwa na mafanikio kwa Yanga, ikumbukwe kambi hiyo ndio iliyomtia adabu Mnyama Simba kuangukia pua katika michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara katika mzunguko wa kwanza na wa pili.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Ofisa Habari wa klabu hiyo, Jerry Muro, alisema matokeo hayo wanayoyatarajia, yatakuja baada ya Yanga kuwa na maandalizi mazuri Pemba kuelekea kwenye mechi dhidi ya Waarabu hao wa Misri.

“Tumeamua kwenda huko kwa kuwa ni sehemu tulivu na mara nyingi tumekuwa tukipata matokeo mazuri tukitokea huko, hivyo tunarajia kupata ushindi.

“Tulipata shida sana, lakini tuliweza kusafiri jana (juzi) na sasa tupo Pemba, wachezaji wataendelea na mazoezi yao kama kawaida tukijiandaa  na ushindi dhidi ya Al Ahly,” alisema Muro.

NA ADAM MKWEPU, MTANZANIA
Yanga ina ari ya kushinda mchezo wa kwanza hapa nyumbani, ili kujiwekea mazingira mazuri ikiwa ugenini.

Gareth Bale - Fast & Furious - Skills & Goals


Sunday, 27 March 2016

CAF: Chad yajiondoa Tz mashakani


Chad imejiondoa kutoka kwenye kinyang'anyiro cha kufuzu kwa dimba la mataifa ya Afrika linalotarajiwa kufanyika mwakani huko Gabon.

Shirikisho la soka la Chad limefikia kauli hiyo kutokana na ukosefu wa fedha.

Katika barua iliyotumwa kwa shirikisho la soka la Tanzania,mwenyekiti wa shirikisho la soka la Chad Moctar Mahamoud, alisema kuwa hawana fedha za kutosha kufadhili safari ya kwenda Dar Salaam kwa mechi ya marudiano dhidi ya Taifa Stars hapo kesho.

CAF imewapiga marufuku Chad kutoka kwenye mashindano ya mwaka wa 2019 mbali na kuitoza faini ya dola $20,000 pesa za Marekani.

Kufuati kujiondoa kwa Chad sasa matokeo ya mechi zote dhidi ya Chad zimefutiliwa mbali na shirikisho la soka la Afrika CAF.

Chad ilikuwa inaburuta mkia katika kundi G.

Tanzania iliyokuwa imeratibiwa kucheza mechi ya marudiano dhidi ya Chad kesho sasa imesalia na pointi 1.

Misri iliyokuwa imeizaba Chad 5-1 sasa ndio wanaongoza kundi hilo wakiwa na alama 4.

Super Eagles ya Nigeria ambao wameratibiwa kuchuana dhidi ya Misri mjini Alexandria siku ya Jumanne sasa sharti washinde alama zote ilikumaliza katika nafasi ya kwanza.

Sheria za CAF zinasema kuwa endapo kundi litakuwa na timu 3 basi timu inayoongoza pekee ndiyo inayosonga mbele.

BBC Swahili