Pages

Friday, 26 February 2016

Kombe la Ligi UK: Kolo Toure amuonya Yaya

Kolo Toure

Yaya Toure

Kolo Toure atakabiliana na nduguye Yaya Toure wakati ambapo Liverpool itakutana na Manchester City katika fainali ya kombe la Ligi ya Uingereza siku ya jumapili katika uwanja wa Wembley.

Lakini beki huyo wa Liverpool anasema kuwa atatumia kila njia kuhakikisha kuwa nduguye hapati bao.

''Ananijua mie kwamba naweza kutumia kila njia kumzuia asifunge bao'',alisema Kolo Toure ambaye ni ndugu mkubwa wa Yaya Toure.

BBC Swahili

Yanga yatangaza raha


WAWAKILISHI wa Tanzania Bara katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Yanga, leo wataikabili Cercle de Joachim ya Mauritius ukiwa ni mchezo wa marudiano hatua ya awali.

Katika mchezo wa kwanza ugenini Uwanja wa George V, Yanga ilishinda bao 1-0, matokeo ambayo yanawapa Yanga kazi nyepesi leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kutinga hatua inayofuata kwani inahitaji angalau sare.

Kocha wa Yanga, Mholanzi Hans van der Pluijm, amejitapa kushinda mchezo huo baada ya maandalizi mazuri waliyofanya kwa wiki mbili tangu warejee nchini.

Pluijm ambaye katika mchezo huo atawakosa nyota watatu wakiwemo wawili wa kimataifa, Haruna Niyonzima na mfungaji wa bao pekee lililowapa ushindi ugenini Donald Ngoma, alisema pamoja na kuhitaji sare, lakini lazima washinde.

“Tumejiandaa vizuri kuhakikisha tunashinda mchezo wa kesho (leo), kwa sababu tumefanya maandalizi ya kutosha na tunacheza nyumbani mbele ya mashabiki wetu hatutapenda kuwaangusha na kizuri zaidi tunawajua vizuri wapinzani wetu,”alisema Pluijm.

Pluijm alisema pamoja na kuwakosa nyota hao, lakini ana imani kubwa na wachezaji waliopo ambao ana hakika watacheza kwa kiwango cha juu na kuwapa ushindi. Wapinzania wa Yanga, Cercle de Joachim, tayari wametua Dar es Salaam kwa ajili ya mchezo huo huku wakionekana wamejipanga kuhakikisha wanalipa kisasi.

Kocha wa timu hiyo, Abdel ben Kacem, amesema amewajua vizuri Yanga na kwa maandalizi waliyoyafanya anaamini atafanikiwa kulipa kisasi. Katika hatua nyingine, kocha wa Simba, Jackson Mayanja, ameitabiria ushindi Yanga katika pambano la leo kwani wapinzani wao ni timu ambayo haina jina kubwa katika soka.

“Sitaki kuizungumzia sana Yanga, lakini nawapa nafasi kubwa ya kushinda mchezo huo, kwa sababu wana timu nzuri na tayari wana akiba ya bao kufuatia ushindi walioupata ugenini, lakini hata timu wanayocheza nayo ni dhaifu,” alisema Mayanja.

MOHAMED AKIDA/HABARI LEO

Ox-lade Chamberlain hatacheza mpira kwa wiki kadhaa kutokana na kuumia goti






Kiungo machachari wa klabu ya Arsenal Alex Oxlade Chamberlain hatocheza kwa wiki kadhaa kutokana na jeraha la goti alilolipata jumanne wakati wa mechi ya  vilabu bingwa Ulaya.

Akiongea na wanahabari Kocha wa Arsenal Arsene Wenger amesema, Chamberlain alipata jeraha walipokabiliana na Javier Mascherano . Jeraha lake ni baya na litamuweka nje kwa wiki kadhaa,''alisema Wenger.

Chambaerlain mwenye umri wa miaka 22  aliondoka  katika uwanja wa Emirates akiwa na magongo.

FIFA election: Gianni Infantino voted new president

  • UEFA general secretary replaces banned Sepp Blatter at the helm of football's world governing body.


Gianni Infantino has been elected as the new president of FIFA, succeeding the banned Sepp Blatter on a term until 2019.

Infantino, the UEFA general secretary, received 115 votes in Friday's second round of voting, more than the required majority of 104 votes from the 207 members.

The other favourite, Sheikh Salman Bin Ebrahim Al Khalifa of Bahrain, had 88 votes.

Prince Ali Bin Al Hussein of Jordan had four and Frenchman Jerome Champagne none.

The 45-year-old former lawyer saluted voters by patting his right hand over his heart, and had to compose himself before starting his acceptance speech.

"We will restore the image of FIFA and the respect of FIFA. And everyone in the world will applaud us," Infantino said, referring to bribery and corruption investigations that have rocked football's governing body and forced Blatter out of office after more than 17 years as president.

"I want to be the president of all of you ... It is time to return to football. FIFA has gone through hard times, crisis times," said Infantino.

"These times are over ... We have to win back the respect, and focus on this wonderful game that is football."

In the first round, Infantino surprising led with 88 votes. Sheikh Salman had 85 votes, Prince Ali 27, and Champagne seven.

Al Jazeera's sports correspondent Lee Wellings, reporting from Zurich, said the pledge of financial support by Infantino to FIFA members might have tilted the balance of votes in his favour.

"Very few people who were at Infantino's manifesto launch felt he could be taking the top job. He put together a good event there and a good campaign," he said.

"What might have been crucial is the pledge of money that Infantino made. But can he back that up by finding that money? We'll see. But that would have made a huge difference because old habits die hard at FIFA."

Infantino is the second straight FIFA president from the Valais region in the Swiss Alps. Infantino is from Brig and replaces the 79-year-old Blatter, who was born in neighbouring Visp.

Blatter was forced out by the pressure of American and Swiss investigations of corruption that hit FIFA two days before the previous election in May.

There were only four candidates on Friday's ballot after Tokyo Sexwale withdrew during his campaign speech to voters, and all four went forward to the second round.

Not since 1974 has a second-round vote been held in a FIFA presidential election.

Then, Joao Havelange of Brazil beat 13-year incumbent Stanley Rous of England 68-52 after an initial 62-56 ballot in Frankfurt, Germany.

Infantino exceeded most observers' expectations after an impressive 15-minute pitch, only 20 minutes before first-round voting began.

The Swiss-Italian spoke in several languages without notes and portrayed himself as a leader for the world, not just his own wealthy confederation.

"We have to get Europe to do much more," Infantino said.

His campaign promised more of key FIFA gifts to member federations: More guaranteed funding from FIFA's $5bn-plus World Cup revenue, more places in an expanded 40-team tournament and more opportunities to stage the World Cup with multi-national regional hosting.

Set of reform passed at Congress

Earlier, the Congress had overwhelmingly passed a set of reforms intended to make FIFA more transparent, professional and accountable.

That package should mean the new president faces much closer scrutiny than Blatter did, and have less influence over the day-to-day management of the organisation's business affairs.

The reforms include term limits for top officials and disclosure of earnings, and a clear separation between an elected FIFA Council responsible for broad strategy and a professional general secretariat, akin to a company's executive board, handling the business side.

Wednesday, 17 February 2016

Makocha watambiana


ZIKIWA zimesalia siku tatu kabla ya pambano la watani wa jadi Simba na Yanga, makocha wa timu hizo wameonesha kuogopana huku kila mmoja akidai kuheshimu kikosi cha mwenziwe.

Yanga imejichimbia Pemba na Simba imejichimbia Morogoro kwa maandalizi ya mechi hiyo ya Jumamosi.

Akizungumza na gezeti hili jana, kocha wa Yanga Hans van Pluijm alisema anafahamu ugumu wa mechi, lakini yeye anaendelea na programu yake ya kusaka ushindi kama kawaida.

“Mimi nakiandaa kikosi changu kwa ushindi kama ilivyo kwenye mechi zote tunazocheza, siandai kikosi changu kwa vile nacheza na Simba, hapana… najua mimi ni bingwa mtetezi nitakutana na ushindani mkubwa lakini nia yangu ni kushinda bila kujali nacheza na nani,” alisema.

Mechi ya mwisho ya ligi ya Yanga ilikuwa dhidi ya JKT Ruvu, ambapo ilishinda mabao 4-0. Pluijm alisema lengo lake ni kuendelea na ushindi.

“Najua kwa sasa ligi ni ngumu sana, kila timu inataka kushinda hasa inapokutana na timu yetu (Yanga) naandaa kikosi changu kushinda, naiheshimu Simba lakini hiyo haifanyi nishindwe kuhakikisha timu yangu inashinda,” alisema.

Kwa upande wa kocha wa Simba, Jackson Mayanja alisema kikosi chake kimejipanga kushinda Jumamosi.

“Tutaingia uwanjani kusaka pointi tatu kama tunavyofanya kwenye mechi zote, mechi ya Yanga tunaichukulia kama ilivyo mechi nyingine yoyote kwenye ligi sasa pointi tatu ni lazima,” alisema.

Tangu kuwa chini ya Mayanja, Simba imekuwa ikipata mfululizo hali iliyorudisha morali kwa wcahezaji na wapenzi wake na kuamini kwamba inaweza kufanya vizuri zaidi na kutwaa ubingwa.

“Kitu kama morali ambacho sikukikuta kwa wachezaji wangu nilipoanza kuwafundisha sasa naona kimerejea na kila mmoja unamwona ana tamaa ya ushindi nami nataka hilo liendelee,” alisema. “Tumeshapanga mikakati yetu na nimewaambia wachezaji wangu kwamba tunacheza mechi ya Yanga sio kutaka kulipa kisasi bali kutaka kupata pointi tatu, na hilo ndilo litakalokuwa,” alisema.

Katika mzunguko wa kwanza timu hizo zilipokutana Yanga ilishinda mabao 2-0.

Habari Leo