Pages

Sunday 27 March 2016

CAF: Chad yajiondoa Tz mashakani


Chad imejiondoa kutoka kwenye kinyang'anyiro cha kufuzu kwa dimba la mataifa ya Afrika linalotarajiwa kufanyika mwakani huko Gabon.

Shirikisho la soka la Chad limefikia kauli hiyo kutokana na ukosefu wa fedha.

Katika barua iliyotumwa kwa shirikisho la soka la Tanzania,mwenyekiti wa shirikisho la soka la Chad Moctar Mahamoud, alisema kuwa hawana fedha za kutosha kufadhili safari ya kwenda Dar Salaam kwa mechi ya marudiano dhidi ya Taifa Stars hapo kesho.

CAF imewapiga marufuku Chad kutoka kwenye mashindano ya mwaka wa 2019 mbali na kuitoza faini ya dola $20,000 pesa za Marekani.

Kufuati kujiondoa kwa Chad sasa matokeo ya mechi zote dhidi ya Chad zimefutiliwa mbali na shirikisho la soka la Afrika CAF.

Chad ilikuwa inaburuta mkia katika kundi G.

Tanzania iliyokuwa imeratibiwa kucheza mechi ya marudiano dhidi ya Chad kesho sasa imesalia na pointi 1.

Misri iliyokuwa imeizaba Chad 5-1 sasa ndio wanaongoza kundi hilo wakiwa na alama 4.

Super Eagles ya Nigeria ambao wameratibiwa kuchuana dhidi ya Misri mjini Alexandria siku ya Jumanne sasa sharti washinde alama zote ilikumaliza katika nafasi ya kwanza.

Sheria za CAF zinasema kuwa endapo kundi litakuwa na timu 3 basi timu inayoongoza pekee ndiyo inayosonga mbele.

BBC Swahili

Cristiano Ronaldo 2015/16 ● Skills & Tricks


Zlatan Ibrahimovic confirms Premier League interest ahead of potential summer move


The Swedish strike ace is out of contract at French side Paris Saint-Germain this summer and has been tipped for a final fling in England

Zlatan Ibrahimovic has admitted he is considering offers to move to the Premier League this summer.

Arsenal have been offered the 34-year-old Swedish superstar while Jose Mourinho will move for Ibrahimovic if he gets the Manchester United job.

Ibrahimovic is out of contract at Paris Saint-Germain this summer and fancies a move to England.

Sweden striker Ibrahimovic, talking ahead if a friendly with Czech Republic, said: "Yes, there is interest from the Premier League, I can confirm that.

"The Premier League is the league in the world all people and fans speak about.

"A lot of things have to feel fine when I'm going to take a decision this summer."

Manchester City and Chelsea could also be interested while Arsenal know Ibrahimovic - currently on around £300,000-a-week - fancies a club in London.

United would be in pole position if Mourinho is installed because the pair are very close and Ibrahimovic wants to link up with him.

Kipa wa zamani wa Simba Dhaira amefariki


Aliyekuwa kipa nambari moja wa timu ya Simba na Uganda Abel Dhaira ameaga dunia.
Dhaira mwenye umri wa miaka 28 alikuwa anaugua saratani.

Dr. Bernard Ogwel, wa shirikisho la soka nchini Uganda FUFA ameithibitishia BBC kuwa kipa huyo alivuta pumzi yake ya mwisho akiwa Iceland.

"Ni jambo la kuhuzunisha sana kuwa Dhaira ametuacha kwetu kama waganda na pia kwa Familia yake''

Dhaira alikuwa amejiunga na klabu ya IBV Vestmannaeyjar ya Iceland alipogunduliwa kuwa anaugua saratani katika miezi ya hivi karibuni.

Kipa huyo alianza kuichezea Uganda Cranes mwaka wa 2009 alipoisaidia timu hiyo kutwaa kombe la CECAFA Senior Challenge 2012.

Afya yake ilidhoofika Januari mwaka huu na akalazwa katika hospitali ya Nsambya kabla ya kurejea Iceland kwa matibabu zaidi.

Kocha wake wa IBV Vestmannaeyjar, Bjarni Johannsson alikuwa ameahidi kumsaidia kwa hali na mali wakati huu anapokabiliwa na maradhi.

Dhaira aliwahi kuichezea Express FC ya Uganda kabla ya kujiunga na AS Vita ya DR Congo na kisha Simba FC ya Tanzania.

BBC Swahili

Ubora, udhaifu Yanga, Azam kimataifa


Dar es salaam. Wakati Yanga na Azam zikijiandaa kukabiliana na vigogo vya soka Afrika kutoka kaskazini mwa bara hilo mwezi ujao, timu hizo zitabebwa au hata kuangushwa na washambuliaji, safu zao za ulinzi zinazohitaji marekebisho makubwa.

Yanga itacheza na Al Ahly ya Misri katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika utakaofanyika Aprili 9 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati Azam itaikabili Esperance ya Tunisia, Aprili 10 kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika (CAF) utakaochezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.

Msimu huu, timu hizo zimeonekana kuwa na safu kali ya ushambuliaji ambazo ni nadra kutoka uwanjani bila bao kwenye mchezo wowote, huku pia zikiwa na viungo mahiri wanaozibeba kwenye mashindano, lakini kama watakuwa kwenye ubora wao.

Yanga inabebwa na washambuliaji, Donald Ngoma, Amissi Tambwe, Simon Msuva na wengineo ambao wamefunga mabao 51 hadi sasa kwenye Ligi Kuu, wakati Azam inaongozwa nao, Kipre Tchetche, John Bocco, Farid Mussa walioiwezesha timu yao kufunga mabao 37.

Waonavyo wadau wa soka
Hata hivyo, baadhi ya wadau wa soka wamekiri kuwa timu hizo zinao uwezo wa kufanya vizuri, ila zinapaswa kurekebisha kasoro ndogo kwenye safu zao za ulinzi ambazo zikiachwa zitawagharimu katika michezo hiyo.

Kocha msaidizi wa JKT Ruvu, Mrage Kabange alisema Yanga na Azam zina soka la kiwango kikubwa, lakini wanapaswa kuongeza juhudi uwanjani katika michezo hiyo, huku wakiamini kila kitu kinawezekana.

Kabange aliyewahi kuichezea Simba na kuzinoa klabu kadhaa nchini alisema timu hizo hazipaswi kuwaogopa wapinzani wao kwani soka la sasa si kama lile zamani ambalo lilikuwa zaidi la mazoea.

Alizitaka klabu hizo kupambana ili kuhakikisha zinaibuka na ushindi katika michezo yao ya nyumbani, zikiamini kuwa ugenini lolote linaweza kutokea, ikiwamo fitina za Waarabu.

“Yanga na Azam zinao washambuliaji wazuri wanaoweza kufunga mabao muda wowote na ubora wa hizo timu unabebwa na aina ya washambuliaji wao, lakini zina matatizo kwenye upande wa mabeki.

“Ukiangalia Yanga, mabeki wake kwanza hawajiamini, wana tatizo la kujipanga, wana papara na wana tatizo kwenye ukabaji na hilo linaweza kuwaletea madhara kwani Waarabu hutakiwi kuwaachia wacheze.

“Pia, Azam nao wana matatizo kwenye upande wa mabeki, angalia hata mechi yao iliyopita dhidi ya Bidvest ya Afrika Kusini, mabeki walizembea, hivyo timu zote zinatakiwa kurekebisha hilo haraka,la sivyo itawagharimu,” alisema Kabange.

Mchezaji wa zamani wa Yanga ambaye kwa sasa ni mchambuzi wa masuala ya michezo, Ali Mayay alisema Yanga inapaswa kupunguza makosa katika safu yao ya ulinzi, huku akiwataka viungo kuongeza umakini.

“Yanga imekuwa na makosa makubwa katika ulinzi, mabeki wao wengi wamepunguza umakini, pia safu ya kiungo nayo inapoteza mipira, hivyo kama wasiporekebisha makosa hayo watapata matatizo mbele ya Waarabu,” alisema Mayay.

Mshambuliaji wa zamani wa Simba, Yanga na Taifa Stars, Zamoyoni Mogella au Golden Boy alisema Yanga na Azam, zote ni timu nzuri lakini zinatakiwa kuwa na nidhamu ya juu ya mchezo ziatakpopambana na Waarabu.

“Siwezi kusema sehemu gani zina upungufu kwani wachezaji wa timu hizo hawana nidhamu ya mchezo, angalia kama Yanga walipokuwa Rwanda walicheza vizuri walipokuja nyumbani mechi ya marudiano walicheza ovyo, sasa wakicheza hivyo mbele ya Waarabu itawagharimu.

“Uzoefu nilionao unapocheza na Waarabu unatakiwa kuwa na nidhamu, kwa sababu timu za huko zinakuadhibu kutokana na makosa unayofanya.

“Azam na Yanga zinatakiwa kuzidisha umakini uwanjani na kusaidiana kwani hata kama eneo fulani mfano ni zuri kama timu haina umakini litaonekana baya,” alisema Mogella.

Oliver Albert, Mwananchi

Thursday 24 March 2016

Zlatan Ibrahimovic - The God - Skills & Goals 2015/16


Michezo ya kufuzu Afcon kuendelea

Kikosi cha Taifa la Ghana

Michezo ya kusaka tiketi ya kushiki michuano ya kombe la mataifa ya afrika mwaka 2017 itayofanyika Gabon itaendelea tena leo

Katika kundi A timu ya taifa ya Djibout itakua nyumbani katika uwanja wake wa Djibouty kukipiga na liberia.

Ghana maarufu kama the Black Stars walioko kundi H watakua wenyeji wa timu ya  Mozambique wanaofahamika kama Mambas.

Comoros watashuka dimbani kuwakabili Botswana huku Madagascar akipimana ubavu na timu ya taifa ya Jamuhuri ya Africa ya kati.

9 things Johan Cruyff did before any other footballer

The legendary Dutchman - who has passed away aged 68 - was not just an awesome footballer. He was an innovative one too

Johan Cruyff was not just an Ajax, Barcelona and Holland legend. He was a football legend.
As one of the greatest talents to ever grace the game, the iconic Dutchman - who has died after losing his battle with cancer - won all manner of awards and medals.
But plenty of famous footballers have retired with bulging trophy cabinets. Cruyff was different. As both a player and a manager, Cruyff was an innovator, often tearing up the rulebook and coming up with new, ground-breaking ways of approaching the game.
Hence why he was the first man in football to do an awful lot of things…
1. First footballer to do THAT turn
How many players have a world famous, regularly used piece of skill named after them?
2. First star of 'Total Football'
Forget tiki-taka. Long before Barcelona and Spain's trademark tactic, there was the Ajax and Holland team of the 1970s and their unique system of "total football". Led by Cruyff, their style was based around quick passing, quick movement and constant rotation of position.
Sound familiar? Cruyff was basically Lionel Messi and Andres Iniesta rolled into one… forty years ago.
3. First player to win three Ballon d'Or awards
Yeah, Messi has five. But long before he was even born, Cruyff won three golden balls in just four years (1971, 1973 and 1974).

4. First man to wear an adidas two-striped shirt in a World Cup final

Perhaps the best evidence of Cruyff's refusal to be conventional came in the 1974 World Cup final, between Holland and West Germany. Holland had a deal with adidas, and so were due to wear the classic adidas three stripes on their shirts for the final.
Cruyff, however, had an individual boot deal with Puma. So, did he diplomatically explain the situation to his sponsors and avoid rocking the boat?
Did he heck. Look closely at the picture above and you'll see that while his team-mates wore the three stripes, Cruyff insisted on only wearing two!
5. First star to regularly wear a squad number outside of 1-11
Johan Cruyff performing the Cruyff turn
All of you young professional footballers who long to wear a bizarre squad number in the 40s or 50s? You owe Cruyff a thank-you.
Back in his day, every team simply wore 1-11. Returning from injury early in the 1970-71 season, the then Ajax forward's No9 shirt was being worn by a team-mate… so he decided he would wear No14.
From then on, he defied convention (not for the first or last time) by sticking with his new number.
6. First footballer to cost $2m
Cruyff's world record moved from Ajax to Barcelona in 1973 made him the first player to cost more than two million US dollars.
Might not sound like much now, but back then that was a FORTUNE.
7. First man to realise the potential of La Masia

La Masia is now a legendary institution - the football factory responsible for the conveyer belt of small, clever, technically gifted players that continue to find their way from into the Barcelona first team.
So where did the idea for football's most famous academy come from? Cruyff, of course.
La Masia existed before he was appointed Barca manager in 1988, but it was a word away from what we know today. Youngsters were picked on size and physical strength. It was Cruyff who changed the outlook, ensuring the emphasis was on technique and ability.
It's no exaggeration to say that without the Dutchman's vision, Andres Iniesta and Lionel Messi may have got no further at Barcelona than the front door.
8. First Dutch international to ever be sent off

Perhaps not the most glorious of his achievements, but against Czechoslovakia in 1968, Cruyff became the first Holland player to ever see red. It was only his second cap.
9. First (and only) winner of European Player of the Century
Which says it all, really…

Adam Johnson afungwa jela miaka sita


Mchezaji soka Adam Johnson amefungwa jela miaka sita kwa kushiriki mapenzi na msichana wa miaka 15.

Jaji Jonathan Rose amesema mchezaji huyo alitumia vibaya nafasi yake na kumsababishia mwathiriwa wake “madhara makubwa ya kisaikolojia”.

Jaji amemwambia Johnson, 28, kwamba alishiriki ngono na msichana huyo akifahamu vyema kwamba alikuwa na umri wa chini ya miaka 16.

Imebainika pia kwamba polisi walipata kanda chafu za video zinazohusisha wanyama kwenye kompyuta mpakato ya Johnson.
Hata hivyo, hatachukuliwa hatua kutokana na hilo.

Mahakama ya Bradford iliambiwa kwamba mchezaji huyo alishiriki mapenzi na msichana huyo katika gari lake aina ya Range Rover Januari 2015.

Johnson alichezea timu ya taifa ya England mara 12. Alikuwa mchezaji wa klabu ya Sunderland.

BBC Swahili

Bao la Samatta laibana Chad, Kenya yachapwa


Bao la Mshambulizi wa Taifa Stars lilitosha kuipa Tanzania ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Chad katika mechi ya kufuzu kwa kombe la mataifa ya Afrika.

Mkwaju wa Samatta kunako dakika ya 30 ya kipindi cha kwanza ilitosha kuipa Taifa Stars ushindi muhimu ugenini.

Kufuatia ushindi huo Taifa Stars ya Tanzania imeimarika na kutoshana nguvu na Nigeria inayoorodheshwa katika nafasi ya pili.

Chad nayo imetokomea ikiburuta mkia katika kundi hilo la G bila alama yeyote.

Nigeria hata hivyo imeratibiwa kuchuana dhidi ya vinara wa ligi hiyo Misri siku ya Ijumaa.
Katika kundi C, Benin ilisajili ushindi mkubwa wa amabao 2-1 ugenini dhidi ya wenyeji wao Sudan Kusini.

Mshambulizi wa klabu ya Uingereza ya West Brom Stephane Sessegnon, alifungua kivuno hicho kunako dakika ya 16 kabla ya kuhakikishia timu hiyo alama tatu muhimu zikiwa zimesalia robo saa mechi hiyo kukamilika.

Kufuatia ushindi huo Benin imejikita kileleni baada ya kuipiku Mali.

Mechi hiyo iliyochezewa Juba ilishuhudiwa na rais mpya wa FIFA Gianni Infantino.

Kenya kwa upande wake itajilaumu yenyewe baada ya kupoteza nafasi nzuri ya kuipiku Guinea nyumbani kwao iliposhindwa bao moja kwa nunge Ugenini.

Harambee Stars ya Kenya ambayo imebadilisha kocha, ilifika Guinea na wachezaji wa nyumbani kabla ya kujiunga na wachezaji wake wa kigeni siku ya mechi.

Kufuatia kichapo hicho Kenya ndio inayoburuta mkia katika kundi hilo bila ushindi wowote.
Vinara wa kundi hilo Zambia na Congo walitoka sare ya bao 1-1.

Katika mechi nyingine Sao Tome na Principe ilitoka nyuma na kuilaza Libya 2-1 katika kundi F.

BBC Swahili

Wednesday 2 March 2016

Chelsea waitumbukiza Norwich hatarini


Norwich wamejipata eneo la hatari Ligi ya Premia baada ya kushindwa na Chelsea wakiwa kwao nyumbani Carrow Road.

Norwich walilazwa 2-1 kwenye mechi hiyo iliyochezwa Jumanne jioni, huku Chelsea wakiendelea kupanda kwenye jedwali chini ya meneja Guus Hiddink.

Beki wa Blues Kenedy alifunga bao kwa kombora alilochomoa akiwa hatua 20 kutoka kwa goli, baada ya sekunde 39 pekee kuchezwa.

Bao hilo ndilo la kasi zaidi kufungwa Ligi ya Premia msimu huu.

Diego Costa aliongeza la pili sekunde chache kabla ya mapumziko, ingawa alionekana kuotea.

Cameron Jerome aligonga mwamba wa goli kabla ya Nathan Redmond kufunga lakini bao lake halikutosha na Norwich walishindwa mechi yao ya nane katika mechi tisa.

Norwich wakishuka eneo la hatari, Chelsea wamepanga kwenye jedwali hadi nambari nane, mara yao ya kwanza kuwa sehemu ya juu ya jedwali tangu wiki ya kwanza ya msimu.

Wameenda mechi 12 ligini bila kushindwa.

Norwich watakutana na Swansea, walio alama tatu juu yao, Jumamosi nao Chelsea wakaribishe nyumbani Stoke siku nne kabla ya kucheza mechi ya marudiano hatua ya 16 bora katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Paris St-Germain.

Matokeo ya mechi za EPL zilizochezwa Jumanne
  • Aston Villa 1-3 Everton
  • Bournemouth 2-0 Southampton
  • Leicester 2-2 West Brom
  • Norwich 1-2 Chelsea
  • Sunderland 2-2 Crystal Palace
BBC Swahili