Pages

Friday 3 June 2016

Manji aivimbia TFF na Baraza la Michezo


Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Yanga anayemaliza muda wake, Yusuf Manji, amegomea mchakato wa awali wa uchaguzi ulioandaliwa na Baraza la Michezo Tanzania (BMT) na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Akizungumza jana kabla ya kuchukua fomu, alisema hawezi kwenda kuchukua fomu za uchaguzi TFF aliodai wanataka kumhujumu.

Akizungumza klabuni hapo, Manji alifichua hujuma mbalimbali zilizokuwa zikipangwa kumhujumu katika mchakato wa uchaguzi uliokuwa chini ya TFF.


Khatimu Naheka, Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here