Pages

Friday 8 January 2016

Mbwana SAMATA aingárisha Tanzania na kuwa Mchezaji bora wa Afrika kwa mwaka 2016



  
   

CAF Africa Award 2016 live; Announcement of The Best African Based Player of the year

Newspaper Review: CAF Awards, 2016 CHAN 07/01/16

Sports This Morning: Discussion On Glo CAF Awards 07/01/16

Mbwana Ally Samata Skills Dribbling Goals 

Mbwana Samata aweka historia ktk soka la Africa

Mshambualiaji wa TP Mazembe ambaye ni raia wa Tanzania  Mbwana Ally Samatta  jana ameingárisha Tanzania baada ya kuchaguliwa kuwa Mchezaji bora wa kiume wa Afrika kwa mwaka  2016.

Samatta ambaye amezungumziwa  kujiunga na KRC Genk ya Ubelgiji akitokea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, amefanikiwa kuweka historia ya kuwa Mtanzania wa kwanza na mchezaji wa kwanza toka nchi za afrika Mashariki kutwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Afrika.

Tuzo hizo zilizofanyika jana usiku nchini Nigeria katika jijini la Abuja,  Samatta aliinuka kidedea na kuwabwagwa mlinda mlango wa TP Mazembe, Robert Kidiaba, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na mshambuliaji raia wa Algeria anayechezea Etoile du Sahel ya Tunisa .

Katika safari yake nchini  Nigeria Samatta   aliambatana na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Selestine Mwesigwa . Mshambuliaji huyo wa Taifa Stars aliifungia klabu yake ya TP Mazembe mabao saba sawa na mshambuliaji wa El Merrikh ya Sudan, Bakri Al-Madina, na kuibuka kinara wa mabao.  Katika tuzo hizo Pierre-Emerick Aubameyang, raia wa Gabon anayechezea Borussia Dortmund ya Ujerumani alitangazwa Mwanasoka Bora wa Afrika 2015 . Nafasi ya tatu katika tuzo ya Mwanasoka Bora Afrika ilimwendea mshambuliaji wa Swansea City ya England raia wa Ghana, Andre Ayew.

Akizungumza baada ya kutangazwa mshindi, Samatta alisema: "Najivunia sana kushinda tuzo muhimu sana kiasi hiki. Najionea fahari na kuonea fahari taifa langu pia. Natoka taifa (Tanzania) ambalo si moja ya mataifa makubwa katika soka Afrika. Kutawazwa kuwa mchezaji bora Afrika, ni jambo kubwa sana kwangu."

Washindi wa tuzo mbalimbali za mwaka huu ni Victor Osimhen (chipukizi bora), Herve Renard (kocha bora), Bakary Gassama (refa bora), Ivory Coast (timu bora ya taifa), TP Mazembe (klabu bora), Cameroon (timu bora ya taifa ya wanawake), Oghenekaro Etebo (kipaji cha mwaka) na Gaëlle Enganamouit (mwanasoka bora wa kike).

Ingawa sherehe ya kutangaza washindi wa tuzo hizo zilifanyika usiku,  Magazeti ya Tanzania yamehakikisha habari za ushindi huo zinatoka ili kuufahamisha ulimwengu juu ya furaha yao kama inavyoonekana hapo juu.

Mwanasoka Bora Afrika

2015    Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon)

2014    Yaya Toure (Ivory Coast)

2013    Yaya Toure (Ivory Coast)

2012    Yaya Toure (Ivory Coast)

2011    Yaya Toure (Ivory Coast)

2010    Samuel Eto’o (Cameroon)

2009    Didier Drogba (Ivory Coast)

2008    Emmanuel Adebayor (Togo)

2007    Frederic Kanoute (Mali)

2006    Didier Drogba (Ivory Coast)

2005    Samuel Eto’o (Cameroon)

2004    Samuel Eto’o (Cameroon)

2003    Samuel Eto’o (Cameroon)

2002    El Hadji Diouf (Senegal)

2001    El Hadji Diouf (Senegal)

2000    Patrick Mboma (Cameroon)

1999    Nwankwo Kanu (Nigeria)

1998    Mustapha Hadji (Morocco)

1997    Victor Ikpeba (Nigeria)

1996    Nwankwo Kanu (Nigeria)

1995    George Weah (Liberia)

1994    Emmanuel Amunike (Nigerua)

1993    Rashid Yekini (Nigeria)

1992    Abedi Pele (Ghana)

Mwanasoka Bora wa Afrika kwa Wachezaji wa Ndani

2015    Mbwana Samatta (Tanzania – TP Mazembe)

2014    Firmin Ndombe Mubele (DR Congo – Vita Club)

2013    Mohamed Aboutrika (Misri – Al-Ahly)

2012    Mohamed Aboutrika (Misri – Al-Ahly)

2011    Oussama Darragi (Tunisia – Espérance)

2010    Ahmed Hassan (Misri – Al-Ahly)

2009    Tresor Mputu (DR Congo – TP Mazembe)

2008    Mohamed Aboutrika (Misri – Al-Ahly)

2007    Amine Chermiti (Tunisia – Étoile du Sahel)

2006    Mohamed Aboutrika (Misri – Al-Ahly)

2005    Mohamed Barakat (Misri – Al-Ahly)


Angalia habari zinazomuhusu Mbwana Ally Samatha

Video na Picha : Kwa Msaada wa Mtandao

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here