Pages

Wednesday 17 February 2016

Chelsea wapigwa bao 2 ugenini


 Zlatana Ibrahimovic na Edison Cavan  (pichani juu) wakishangilia ushindi baada ya kuifungia timu yao bao la kwanza na la pili


Klabu ya Paris St-Germain ya Ufaransa jana ilijipatia ushindi dhidi ya Chelsea  katika mechi ya moja ya mzunguko wa  Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya .

Siku ya jana ilikuwa mbaya kwa Chelsea  na hadi mwisho wa mchezo waliishia kuchezea kichapo cha  mabao 2-1 .

Paris St-Germain walikuwa wa kwanza kuliona goli la Chelsea  katika dakika ya 39 kupitia mshambuliaji hatari  wa Sweden Zlatan Ibrahimovic .

Kupitia Mikel Obi  ndani ya dakika ya 45 Chelsea nao walifanikiwa kusawazisha  lakini furaha yao ilizimwa katika dakika ya 78  baada ya Edison Cavan  kuongeza bao la pili  bao ambalo lilidumu hadi mwisho wa mchezo na kuwafanya PSG wawe washindi kwa mechi ya jana.


Picha : Mirror

Picha zaidi kuhusu mechi hii fungu hapa

0 comments:

Post a Comment

Want to comment? write down here